EURO 2012: MAKUNDI KUMALIZIKA USIKU HUU, ENGLAND V UKRAINE!!
Leo Usiku huko Nchini Ukraine, ambao ni Wenyeji wenza wa Fainali za EURO 2012 pamoja na Poland, zitachezwa Mechi za mwisho za Makundi kwa Mechi mbili za Kundi D ambako Wenyeji Ukraine wataingia dimbani kucheza na England Uwanja wa Donbass Arena Mjini Donetsk, Ukraine na France watacheza na Sweden Uwanja wa Olimpiki Mjini Kiev, Ukraine.
Wakati Sweden wameshaaga Mashindano, Ukraine, France na England bado zipo kwenye kinyang’anyiro kuwania nafasi mbili kuingia Robo Fainali ili kucheza na Mabingwa Watetezi Spain au Italy ambao walifuzu jana.
RATIBA
Jumanne, Juni 19
KUNDI D
Saa 3 Dak 45 Usiku
Donetsk, Ukraine
England v Ukraine
Kiev, Ukraine
France v Sweden
No comments:
Post a Comment