BUKOBA SPORTS

Tuesday, June 19, 2012

KENYA YAMTIMUA KOCHA WA TIMU YA TAIFA FRANCIS KIMANZI


Kimanzi alikuta barua ya kufukuzwa kazi inamsubiri muda mchache baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta akitokea Togo, alipoenda kuiongoza Harembee Stars kucheza dhidi ya Togo na kufungwa kwa bao 1-0, hivyo kupelekea timu hiyo kupoteza matumaini ya kucheza michuano ya African Cup of Nations in 2013.

Mbadiliko hayo yamehitimisha utawala wa Kimanzi ambaye aliingia Harembee tangu November 1, 2011, akichukua nafasi ya Zedekiah Otieno Zico.
Lakini katika makubaliano ya kusitisha kibarua chake, Kimanzi amakubaliana na KFF kwamba atashushwa cheo na kuwa mkurugenzi wa ufundi huku nafasi ya ukocha kwa sasa ikiwa ipo wazi.

No comments:

Post a Comment