BUKOBA SPORTS

Wednesday, September 26, 2012

CAPITAL ONE CUP KIPIGO CHA MAN CITY KUONDOLE JANA - MANCINI AMVAA MENEJA WA VILLA PAUL LAMBERT!

Bosi wa Manchester City Roberto Mancini jana, mara baada ya Timu yake kuchapwa 4-2 na Aston Villa na kutolewa nje ya Mashindano ya CAPITAL ONE CUP, amesema kuwa amechoshwa na tabia za Mameneja wa Timu pinzani na hilo limekuja baada ya kukwaruzana na Meneja wa Aston Villa Paul Lambert wakati wa Mechi hiyo.
Hata hivyo, Paul Lambert amesema: “Kulikuwa hamna kitu. Kama kasema maneno yeyote mie sijali. Namuheshimu kama Kocha na Mchezaji wa zamani. ”
Mancini alimpandishia Lambert mara baada ya Mchezaji wa Villa Joe Bennett kumparamia Kiungo wa Man City Gareth Barry.
Mancini ameeleza: “Nilimuuliza Refa wa Akiba kama ipo Kadi ya Njano bila kuonyesha ishara kwa mikono kuonyesha Kadi na yeye Lambert akanifuata mimi. Sikuwa naongea nae sasa kwa nini anifuate.”
Aliongeza: “Nimechoshwa na hizi tabia zao. Wengine wakienda Viwanja vikubwa hawasemi kitu. Mbona wakiwa Old Trafford hawasemi kitu?”

MIGONGANO YA MANCINI na Mameneja wenzake:
=Sir Alex Ferguson - April 2012: Walivaana na ilibidi watenganishwe kwenye Mechi iliyochezwa Uwanja wa Etihad.
=Mark Hughes - Feb 2011: Mabishano yalizuka kuhusu kupeana mkono mwisho wa Mechi na Mark Hughes Meneja wa Fulham alietimuliwa Man City na nafasi yake kuchukuliwa na Mancini.
=David Moyes - March 2010: Mancini alipigwa Faini  £20,000 na FA baada ya kupatikana na hatia ya kumsukuma Meneja wa Everton David Moyes wakati wa Mechi akidai anachelewesha mpira wakati alipoudaka mpira uliotolewa nje.

Katika Mechi hiyo ya jana na Aston Villa, Man City mara mbili waliongoza kwa Mabao ya Mario Balotelli na Aleksandar Kolarov alakini Villa wakasawazisha kwa Bao la kujifunga mwenyewe Barry na jingine la Gabriel Agbonlahor.
Kisha Charles N'Zogbia na Agbonlahor  wakapiga Bao mbili katika Dakika 30 za nyongeza na kuwatupa nje ya CAPITAL ONE CUP na pia kuwafanya Mabingwa hao wa England wawe hawajashinda katika Mechi zao 4 hadi sasa.

No comments:

Post a Comment