BUKOBA SPORTS

Tuesday, September 11, 2012

KIRAFIKI: NEYMAR NOMA APIGA HAT- TRICK BRAZIL 8 CHINA 0, OSCAR NA RAMIRES WAMALIZIA !!



Three and easy: Neymar scored a hat-trick in Brazil's thumping win over China LEO Alfajiri huko Estadio Jose do Rego Maciel, Recife, Pernambuco, Brazil, Supastaa wa Brazil, Neymar, ambaye Ijumaa alizomewa na Mashabiki baada ya Brazil kuifunga South Africa 1-0 huku yeye akidorora, amefunga Bao 3 Brazil ilipoichapa China Bao 8-0 katika Mechi ya Kirafiki.Oscar akifunga penati akiipigia penati brazil kushinda 8-0 dhidi ya China

Hii inakumbusha mwaka 2008 kwa hizi goli 8 Samba alivyofanya vituzz..
MAGOLI YA  BRAZIL
′ Ramires dk 23
′ Neymar dk 26
′ Lucas dk 49
′ Hulk dk 52
′ Neymar dk 54
′ Neymar dk 60
′ (Kajifunga mwenyewe) Jianye Liu dk 70
′ Oscar dk 76
Tofauti na kwenye Mechi na South Africa, leo Brazil walikuwa hawakamatiki na kila idara ilicheza kwa umahiri mkubwa hasa Neymar na Kiungo mpya wa Chelsea Oscar ambao ndio walikuwa nguzo kubwa ya ushindi huo mkubwa.
Akielezea kutofurahishwa kwake na kuzomewa na Mashabiki wa Brazil, Neymar alisisitiza: “Mimi si mashine!”
Neymar, Mwenye Miaka 20 tu, amedokeza kuwa huenda Mashabiki wanategemea vitu vikubwa toka kwake na amesema: “Nilijisikia naumwa kwa yale yaliyotokea kwenye Mechi na Afrika Kusini. Mie sio mashine. Nilijisihi kuchoka baada ya Mechi na Afrika Kusini, kimwili na kiakili. Nataka niendelee kucheza tu na kuisaidia Santos na Brazil!”vijana wa Brazil wakishangilia ushindi usiku wa kuamkia leo baada ya kuitwanga goli 8-0 chinaBRAZIL-RECIFE-SOCCER-BRA VS CHNkikosi kilichoiangushia kilio china leo hii.

kwa hisani soka in bongo

No comments:

Post a Comment