MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson yuko tayari kutimiza ndoto za mwanariadha nyota wa mbio fupi kutoka Jamaica kwa kumjumuisha katika kikosi chake ambacho kinatarajia kucheza mchezo wa hisani dhidi ya Real Madrid. Bolt mwenye umri wa miaka 25 alinyakuwa medali mbili za dhahabu katika mbio za mita 100 na 200 kwenye michuano ya Olimpiki iliyofanyika Agosti jijini London na baadae kumuomba Ferguson kumfanyia majaribio katika klabu yake. Ferguson alimjibu nyota huyo ambaye ni shabiki wa kutupwa wa klabu hiyo kwa kumualika kama mgeni rasmi katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza dhidi ya Fulham mwishoni mwa mwezi uliopita na kutambulishwa kwa mashabiki pamoja na wachezaji wa timu hiyo. Bolt ambaye aliweka rekodi mpya katika mbio za mita 100 kwa kutumia muda wa sekunde 9.63 katika Uwanja wa Olimpiki uliopo katika mji wa Stratford maombi yake ya kufanya majaribio yanaonekana kufanikiwa.
Usain Bolt, ambae ni Mtu mwenye mbio za kasi kupita Binadamu yeyote Duniani, ataichezea Manchester United katika Mechi ya Kirafiki na Real Madrid Msimu ujao.
Mara tu baada ya kunyakua Medali za Dhahabu kwenye Michezo ya OLIMPIKI LONDON 2012, Usain Bolt alikuwa mgeni wa heshima kwenye Mechi ya Ligi Kuu England Mwezi uliopita iliyochezwa Old Trafford wakati Manchester United ikiifunga Fulham Bao 3-2 na Bingwa huyo aliwataka Mashabiki wa Man United wamsisitize Sir Alex Ferguson ili amsaini yeye kama Mchezaji.
Na sasa inaelekea ndoto ya Bolt kuichezea Man United huenda ikatimia baada ya Meneja wa Man United, Sir Alex Ferguson, kudokeza kumwalika Bingwa huyo kucheza Mechi ya Kirafiki na Real Madrid.
Ferguson amesema: “Bolt ni Mtu jasiri na mpenzi mkubwa wa Man United. Inavutia akisema anataka kuichezea Klabu hii. Mwakani tunaweza kumwita acheze Mechi ya Kirafiki na Real.”
Bolt, Miaka 25, ameshawahi kufanya mazoezi na Man United.
Mechi hiyo ya Kirafiki na Real Madrid imepangwa Tarehe 3 Juni 2013 na, na kama ilivyofanywa Mwezi mmoja uliopita ilipochezwa huko Santiago Bernabeu, Mechi hiyo ambayo itachezwa Old Trafford, itawashirikisha Wachezaji Maveterani waliowahi kuchezea Klabu hizo Kongwe.
Bolt akicheza uwanjani kuonyesha cheche zake.

Manchester united itakavyojipanga ikiwa na Usain Bolt
Akihojiwa na gazeti la timu hiyo Ferguson amesema kuwa alizungumza na Bolt na kumuuliza kama anaweza kucheza mechi ya hisani na akamjibu kwamba anaweza, hivyo itakuwa ni jambo zuri kumtumia katika mchezo wa hisani dhidi ya Madrid ambao utapigwa Januari mwakani na kumuangalia kama ataweza.

Mafans wa Bolt ... Kingston, Jamaica wakifatilia mtanange Bolt aliposhinda
100m champ ... Usain Bolt
No comments:
Post a Comment