USAHILI WA WASANII WA FILAMU ZACHWA INVESTMENT COMPANY L.T.D ULIOFANYIKA JANA TAREHE 9/9/2012 KATIKA UKUMBI WA BARAKA JUHUDI - HAMUGEMBE BUKOBA
Wasanii wa filamu walijitokeza kwa wingi jana na ilikuwa mara ya kwanza kwa usahili huo unaofanywa na kampuni ya Zachwa Investment ya hapa Bukoba, Ambapo mchujo ulifanyika na takribani wasanii waliokuwa wamejitokeza ni 58 na kuchujwa kubaki 42. Niliongea na Chief Judge Bi.Regina hiyo jana jioni na kuniambia kuwa usahili utaendelea na hao 42 waliopatika pia watachujwa na kupata wasanii wazuri zaidi wa kuja kufanya filamu bora na nzuri zaidi na ya kisasa hapa nchini Tanzania na duniani kote.Vigezo na masharti vilizingatiwa na baadhi vilichekiwa vitu vifuatavyo katika mchujo huo uliokuwa mgumu ni Rafudhi, kujiamini/confidence, muonekano, Experience, kipaji na personality(VTU) katika usahili huo. wasanii wakiingia ndani kwenye ukumbi wa Baraka uliopo eneo la Hamugembe Wasanii mbalimbali wakiingia katika ukumbi wa Baraka Juhudi Wasanii wakiingia katika ukumbi wa Baraka Juhudi Mkurugenzi mkuu wa Zachwa Investment Bw. Muganyizi (kushoto) ambaye ndiye Mdhamini mkuu na (kulia) ni Bi. Regina ambaye ndiye Chief Judge wa shindano hili la wasanii. Bw. Slay (kushoto) Na Bi. Abera(kulia) watangazaji wa Radio ya Kasibante Fm iliyopo Bukoba wakiwa meza kuu wakiendelea kuangalia usahili huo wao walikuwa ni ma JudgeBwana Hamad sudi Katabalo - mwigizaji na mwalimu mwongozaji akitoa neno kwa wasahili jana Baadhi ya wananii waliojitokeza kuwania nafasi hiyo wasanii wakiendelea kusikiliza ma judge katika usahili huo uliofanyika jana tarehe 9/9/2012 wasanii wakiwa nje na kupeana neno hapa na pale kuhusu usahili huo wasanii wakitokelezea kwenye picha mara baada ya kuniona na kutaka ukodak muda huo. WA COMEDY NAO WALIKUWEPO wasanii wakielekeza jambo nje ya ukumbi..Ndugu Tesso Boy (kushoto) akizungumza na rafiki yake baada ya kukutanishwa na usahili wa filamu kwa pamoja wasanii walianza kuoneshana mbwembwe za uigizaji kila mmoja akionesha makeke yake
kuigiza kwenye filamu si swala la mchezo kila mtu ana nafasi yake katika kuigiza, awe ni mtu mzima, mtoto, kijana ..wanayo nafasi.
No comments:
Post a Comment