BUKOBA SPORTS

Thursday, September 6, 2012

ZENIT WAJIANDAA KUMNUNUA NANI NA ANDREY ARSHAVIN KABLA YA DIRISHA LA USAJILI LA URUSI KUFUNGWA LEO HII


Mchezaji wa timu ya Manchester United Nani anasubiri kujua hatima yake leo kama atauzwa na United kwenda klabu ya Zenit St Petersburg kabla dirisha la Usajili la Urusi halijafungwa leo.

Nani alitarajiwa kusaini mkataba mpya na Man United ili aweze bakia klabuni hapo kwa mda mrefu lakini jambo hilo limeshindika kwani hapakuwa na maelewano mazuri katika mkataba huo na kupelekea Nani kujiona haitajiki klabuni hapo na pia inasemekana hayupo katika mipango ya kocha Ferguson.
Zenit Pia wameushangaza ulimwengu wa soka baada ya kutoa paundi mil 70 kwa ajili ya kuwasajili mshambuliaji wa Porto Hulk na kiungo wa Benfica Axel Witsel na inasemekana wanataka toa paundi mil 25 kwa ajili ya kumpata Nani.
Hulk
Vilevile inasemekana Zenit wanataka kumrudisha Arshavin katika klabu hiyo kabla dirisha halijafungwa.

Andrey Arshavin

No comments:

Post a Comment