BUKOBA SPORTS

Sunday, October 14, 2012

KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE. (BABA WA TAIFA)

Hapo hakuna Udini, Ukabila, Urafiki wala Ushikina; kutoka kushoto ni Marehemu Habib Halala, Mzee Paul Soizgwa, JK Nyerere, Brig. Hashim Mbita, Mzee Mkapa, siku kumi kabla ya JK kustaafu uraisi 1985.

Leo ni kumbukumbu ya Baba waTaifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Waziri Mkuu na Rais wa kwanza wa Tanzania (13 Aprili 1922 – 14 Oktoba1999) 
Hayati Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julias Kambarage Nyerere
Afikisha Miaka 13 Tangu Kifo Chake
JULIAS Kambarage Nyerere alizaliwa mwaka 1922 (katika kijiji cha Butiama, wilaya ya Musoma, Mkoa wa Mara, Tanzania (wakati ule: Tanganyika). Alikuwa mojawapo kati watoto 26 wa Nyerere Burito, chifu wa kabila la Wazanaki. Alipokuwa mtoto Nyerere alichunga mifugo ya babake; katika umri wa miaka 12 aliingia shule akitembea kilomita 30 hadi Musoma. Baada ya kumaliza shule ya msingi aliendelea kusoma shule ya wamisionari Wakatoliki huko Tabora. Katika umri wa miaka 20 alibatizwa akawa mkristo Mkatoliki hadi mwisho wa maisha yake.
Mapadre wakaona akili yake wakamsaidia kusoma ualimu huko Makerere, Kampala, Uganda kuanzia 1943 – 1945. Makerere akaanzisha tawi la Umoja wa wanafunzi Watanganyika pia amejihusisha na tawi la Tanganyika African Association (TAA). Baada ya kumaliza masomo ya ualimu alirudi Tabora akifundisha shule ya St. Mary´s. Mwaka 1949 alipata skolashipu ya kwenda kusoma kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh huko Uskoti / Uingereza akasoma M. A. ya historia na uchumi (alikuwa mtanzania wa kwanza kusoma katika chuo kikuu cha Uingereza na mtanzania wa pili kupata shahada ya elimu ya juu nje ya Tanzania).
Aliporejea Tanganyika kutoka masomoni, Nyerere alifundisha Historia, Kingereza na Kiswahili katika shule ya St. Francis iliyo karibu na Dar es Salaam. Mwaka 1953 alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African Association (TAA), chama ambacho alikisaidia kukijenga alipokuwa mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Makerere. Mwaka 1954 alikibadilisha chama cha TAA kwenda katika chama cha Tanganyika African National Union (TANU) ambacho kilikuwa cha kisiasa zaidi kuliko TAA. Ndani ya mwaka mmoja chama cha TANU kilikuwa tayari chama cha siasa kinachoongoza Tanganyika.
Uwezo wa mwalimu Nyerere uliwashitua uongozi wa kikoloni na kumlazimisha Nyerere kuchagua kati ya siasa na kazi ya ualimu. Nyerere alisikika akisema kuwa alikuwa mwalimu kwa kuchagua na mwanasiasa kwa bahati mbaya. Alijiuzuru ualimu na kuzunguka nchini Tanganyika kuzungumza na watu wa kawaida na machifu ili kuleta muungano katika mapigano ya uhuru. Pia alizungumza kwa niaba ya TANU katika Trusteeship council na Fourth committee ya Umoja wa Mataifa (UN) huko New York.
Uwezo wake wa kimaongezi na kuunganisha watu ulimwezesha kufanikisha Tanganyika kupata uhuru bila umwagaji wa damu. Ushirikiano mzuri aliouonyesha aliyekuwa gavana wa wakati huo bwana Richard Turnbull ulisaidia pia kuharakisha upatikanaji wa uhuru. Nyerere aliingia katika bunge la kikoloni mwaka 1958 na kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mwaka 1960.
Mwaka 1961 Tanganyika ilipata uhuru wake na Desemba 9, 1961 Nyerere alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika huru na mwaka mmoja baadae Nyerere alikuwa raisi wa kwanza wa Jamhuri ya Tanganyika. Nyerere alikuwa kiungo muhimu katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania baada ya mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 yaliyomtoa madarakani sultani wa Zanzibar Jamshid bin Abdullah.
Februari 05, 1977 aliongoza chama cha TANU katika tendo la kuungana na chama tawala cha Zanzibar ASP na kuanzisha chama kipya cha CCM (Chama cha Mapinduzi) akiwa mwenyekiti wake. Nyerere aliendelea kuongoza Taifa hadi 1985 alipomwachia nafasi raisi wa pili Ali Hassan Mwinyi. Aliendelea kuongoza Chama cha CCM hadi 1990 na kuwa na athari kubwa katika siasa ya Tanzania hadi kifo chake.
Julius NyerereInasadikika kuwa Nyerere alishawishi uteuzi wa Benjamini W. Mkapa kama mgombea wa raisi wa mwaka 1995 na ambaye aliteuliwa kuwa raisi kwenye uchaguzi wa mwaka 1995. Nyerere alikaa muda mwingi kwake Butiama akilima shamba lake. Pamoja na haya alianzisha taasisi yenye jina lake; mwaka 1996 alionekana akiwa mpatanishi wa pande mbalimbali wa vita vya wenyewe kwa wenyewe huko Burundi. Oktoba 14, 1999 aliaga dunia katika hospitali ya St. Thomas London baada ya kupambana na kansa ya damu.
Sote tunaweza kuwa maarufu, tunaweza kuwa chochote tunachotaka . Pamoja na hayo, jambo moja ambalo ni dhahiri itakuwa ni vigumu sana kulifikia ni kuwa maarufu na kuheshimika duniani kote kama ilivyokuwa kwa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye hivi leo tunakumbuka miaka kumi na moja (11) tangu afariki dunia mnamo tarehe kama ya leo mwaka 1999 kule nchini Uingereza katika hospitali ya Mtakatifu Thomas kwa ugonjwa wa saratani ya damu (leukemia).
Serikali ilipotangaza rasmi kwamba Nyerere hatunaye tena, uchungu na simanzi uliikumba nchi nzima na dunia kwa ujumla hususani kwa wale waliokuwa wanamjua Nyerere na kujua alichokuwa akikisimamia na alichokiamini. Bara la Afrika likawa limempoteza kipenzi chake, mtoto wa Afrika ambaye thamani ya mchango wake katika ukombozi wa bara la Afrika haina kipimo. Mpaka anafariki dunia alikuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha amani barani Afrika.Mfano mzuri ni mgogoro wa Burundi aliokuwa akijaribu kuusuluhisha. Mwenyewe aliwahi kutamka kwamba yeye ni mwafrika kwanza na kisha mjamaa.
Julius Kambarage NyerereMpaka leo hii jina la Nyerere linabakia kuwa kitambulisho chetu kikubwa .Wakati mwingine zaidi hata ya jina la nchi yetu yaani Tanzania.Wapo watu wanaolijua jina la Nyerere na wala wasijue jina la Tanzania au hata Tanganyika. Haishangazi, alikuwa ni mwana wa Afrika kamili. Kadiri siku zinavyopita, taratibu baadhi yetu, hususani vijana wanaoitwa wa kizazi kipya, wanazidi kulisahau jina la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Viongozi wetu wengi wa sasa( ingawa wakati wa msiba wake waliahidi kumuenzi kwa hali na mali) wanaelekea kusahau kabisa ahadi zao! Wengi wanabakia kumuenzi kwa maneno na sio vitendo.
Lakini je,sote tunafahamu japo kidogo tu historia ya Mwalimu Nyerere? Uwezekano ni kwamba sio wote,hususani vijana wa sasa. Kwa kifupi na kwa msaada wa vyanzo mbalimbali hii hapa historia fupi ya Hayati Baba wa Taifa;
Nyumba aliyojengewa Mwalimu Nyerere na serikali baada ya kustaafu.Ipo Butiama. 

WWW.BUKOBASPORTS.COM TUTAKUKUMBUKA DAIMA!!!


 Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alizaliwa tarehe 13 Aprili mwaka 1922 huko Butiama mkoani Mara, pembezoni mwa ziwa Victoria,kaskazini mwa Tanzania. Baba yake alikuwa ni Chifu katika kabila dogo la Wazanaki.Nyerere alikuwa miongoni wa watoto wanaosemekana kufikia hadi 26. Baba yake, Mzee Burito Nyerere alikuwa na wake wapatao 22.Alianza shule akiwa na umri wa miaka 12 (ilimbidi kutembea kwa zaidi ya kilometa 26 hadi Musoma mjini ili kupata elimu ya msingi). Kipaji cha uelewa shuleni kilimuwezesha kumaliza kozi ya miaka minne ndani ya miaka mitatu tu. Baadaye mnamo mwaka 1937,alijiunga na shule ya sekondari ya serikali ya Tabora kwa masomo ya sekondari. Alibatizwa katika kanisa katoliki akiwa na umri wa miaka 20.
Kipaji chake cha kitaaluma na kiuongozi kilionekana tangu mapema. Kwa msaada wa waliokuwa waalimu wake pale Tabora (ma-father wa kanisa katoliki) baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda kusomea ualimu. Fikra za kimapinduzi na kusaidia waafrika wenzake zilianza kuonekana wazi akiwa Makerere.
Baada ya kumaliza Makerere alirejea Tanzania na kwenda kufundisha (St. Mary’s Secondary School) mkoani Tabora. Mwaka 1949 alipata scholarship kwenda Chuo Kikuu cha Edinburgh kusomea shahada ya pili (Masters) katika historia na uchumi wa kisiasa(History and Political Economy). Alipokuwa masomoni Edinburgh, Nyerere ndipo alipoanza rasmi kuunda mawazo yake ya kiukombozi kufuatia kuanza kujifunza kilichoitwa Fabian Thinking . Mawazo yake ya kuunganisha ujamaa na ujima au maisha ya kijamii ya kiafrika ndipo yalipoanza kujijenga au kujiimarisha.Harakati za kujipatia uhuru kwa nchi ya Ghana zilizokuwa zikiongozwa na Dr.Kwame Nkrumah,anakiri Nyerere katika baadhi ya mahojiano aliyowahi kufanya, zilichangia kuamsha fikra za kujikomboa kutoka mikononi mwa wakoloni. Inasemekana Nyerere ndio alikuwa mtanzania wa kwanza kusomea katika chuo kikuu cha Uingereza na mtanzania wa pili kupata degree nje ya Afrika. Alihitimu mwaka 1952.
Aliporejea nchini Tanzania (enzi hizo bado ikiitwa Tanganyika), alianza kazi ya kufundisha masomo ya Historia, Kiingereza na Kiswahili katika shule ya St.Francis’ (sasa Pugu Sekondari). Wakati huo huo akawa amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa TAA(Tanganyika African Association) chama kilichokuwa kimeundwa kusimamia maslahi ya waafrika ingawa tayari kikiwa na vuguvugu la kiukombozi na kisiasa. Hapo ndipo serikali ya kikoloni ilipomlazimisha kuchagua kati ya kufundisha(ualimu) au siasa. Mwenyewe anasema alikuwa amepanga kufundisha kwa angalau miaka mitatu kwanza kabla ya kuingia moja kwa moja kwenye siasa. Hilo halikuwezekana. Akachagua kuwa mwanasiasa na hivyo kuanza mkakati mzito wa kuviunganisha vyama mbalimbali vilivyokuwa na malengo sawa.

Kazi ya kuviunganisha vikundi mbalimbali vya kisiasa vilivyokuwa vimeanza kutapakaa nchi nzima haikuwa rahisi. Lakini alifanikiwa kufanya hivyo mwaka 1954 kwa kuundwa kwa TANU(Tanganyika African National Union) na yeye kuchaguliwa kukiongoza.
Humo ndimo alimopumzika Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere.Tizama na tafakari kwa makini maneno yaliyoandikwa hapo nje.
Aliingia katika bunge la wakati huo mwaka 1958 kabla hajawa waziri mkuu mwaka 1960. Tarehe 1 May 1961, Tanganyika ilipewa uhuru wa kujitawala na Nyerere akawa waziri mkuu wa kwanza. Uhuru kamili ulipatikana mwaka tarehe 9 December 1961. Mwaka mmoja baadaye (1962) Nyerere akawa Raisi wa kwanza wa Tanganyika ilipokuwa Jamhuri ya Tanganyika.
Nyerere,mama yake na mkewe
Mwalimu Nyerere(katikati),mama yake mzazi(kushoto) na mkewe Maria(kulia).Picha hii ilipigwa Novemba 10,1985 Butiama baada ya Nyerere kustaafu.
Julius Nyerere alimuoa Maria Gabriel Magige (Mama Maria Nyerere) tarehe 24 Januari 1953 na walijaliwa kupata watoto wanane. Alipostaafu nafasi yake ya uraisi mwaka 1985 alirudi kijijini Butiama ambako alibakia kuwa mkulima wa kawaida mpaka kufariki kwake Oktoba 14, 1999. Endelea kupumzika kwa amani Mwalimu.
Tanzania note
Sura ya Nyerere katika noti ya Shs 100 enzi hizo.
R.I.P MWALIMU JULIUS K.NYERERE.

Kila tarehe 14/10 wanajumuiya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hujumuika na Watanzania wengine kote nchini kumkumbuka muasis wa taifa la Tanzania, hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Maadhimisho ya mwaka huu yalikuwa ni ya nane tangu Mwalimu kututoka. Kama ilivyo ada mwaka huu pia watu wamekusanyika tena katika ukumbi maarufu wa Nkrumah pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutimiza azma yao.
  ____________________________________________________

NANI ALIKUWEPO KUMKUMBUKA MWALIMU?

Dakta Salim Ahmed Salimu, aliyewahi kuwa katibu mkuu wa OAU na sasa mwenyekiti (kama sijakosea) wa Taasis ya Mwalimu Nyerere alikwepo kumuenzi Mwalimu. Kumbuka Salim aliwahi kupewa kazi ya kuliwakilisha taifa kimataifa angali kijana mdogo kabisa wa miaka kumi na tisa tu. Pembeni ya Dakta Salim ni balozi wa Afrika ya Kusini, kumbuka pia kuwa Afrika Kusini ina deni kubwa sana la fadhila kwa Tanzania kutokana na msaada wa hali na mali Tanzania iliyoipatia Afrika ya Kusini kipindi kile cha vita dhidi ya ubaguzi wa rangi, ndio maana balozi yuko hapa.


JENERALI ULIMWENGU NA KAZI ZA MWALIMU


Jenerali Ulimwengu anapewa nafasi ya kuzungumzia kazi za Mwalimu Nyerere. Anaanza kwa kusema huwezi kuzungumzia kazi za Mwalimu katika muda wa dakika thelathini ambazo waratibu wa kumbukumbu hii wamempatia. Anasema atakachozungumzia yeye ni kama dibaji tu ya kazi za Mwalimu.

Anaanza kwa kusema kuwa ukitaka kuzungumzia kazi za Mwalimu ni lazima kichwani kwako uelewe kuwa Mwalimu alikuwa ni mtu mwenye kupenda kubadilika, anasema hadi Mwalimu anafariki katika umri wake mkubwa aliokuwa nao, akili yake bado iliweza kufikiri kileo. Anatoa mfano kuwa wakati kuna watu wengi ndani ya CCM, ambacho kilikuwa ni chama cha Mwalimu hadi mauti yanamkumba, kilikuwa kikipinga kabisa kabisa ujio wa sera ya vyama vingi, Mwalimu hakuona aibu kusimamia kidete ujio wa mabadiliko yale kwani alikwishaona wimbi la mabadiliko yaliyokuwa yakitokea ulimwenguni. Jenerali anasema kuwa, “Usisahau kuwa Mwalimu alikuwa ni kiongozi wa kwanza kufutilia mbali mfumo wa vyama vingi hapa nyumbani lakini muda wake ulipopita hakuona haya kusema kuwa jitayarisheni kwa mabadiliko.” 

PROFESA ISSA SHIVJI ALIVYOMKUMBUKA MWALIMU

062.JPG
Tumerudi kwenye ngwe ya pili ya kumjadili Mwalimu baada ya mapumziko mafupi. Wa kwanza anayepewa nafasi ya kumzungumzia Mwalimu kwa sasa ni mhadhiri wa Sheria wa siku nyingi, Profesa Issa Shivji. Shivji pia ni mmoja wa Wajamaa wachache waliosalia wanaoishi katika jamii ya kibepari. Kwa wale wenye tatizo na Richa Adhia, mrembo wa Tanzania 2007, nadhani watakuwa na tatizo pia na uhalali wa u-Tanzania wa mhadhiri huyu. Haituhushu kwa sasa tuendelee.

Katika kumjadili Mwalimu, Shivji anaanza kwa kusema, “Huu si tu mwaka wa 8 toka Mwalimu kufariki bali pia ni mwaka wa 40 tangu kuzaliwa kwa Azimio la Arusha. Mbona wote tumesahau basi kukumbuka kuuawa pia kwa Azimio? Hata Taasisi ya Mwalimu pia imesahau hilo, ingekumbuka ingetutahadharisha katika kutengezeza kauli mbiu ya kumkumbuka Mwalimu na marehemu mwanae, Azimio la Arusha.”



WWW.BUKOBASPORTS.COM TUTAKUKUMBUKA DAIMA!!!

No comments:

Post a Comment