sir Alex Ferguson
MANCHESTER, England
“Matokeo ya leo usiku
yanatuweka sisi mbali kidogo na Chelsea
katika mbio za ubingwa wa ligi. Sisi bado tuko mbele tukiongoza msimamo wa
ligi, lakini Man City wako karibu yetu na msimu bado ni
mrefu”
KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amekenulia
meno mwanzo mbaya wa kocha wa Chelsea, Rafa Benitez klabuni Stamford Bridge,
na kutabiri ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu ni kinyang’anyiro cha timu za jiji la
Manchester.
Chelsea inayoshikilia ubingwa
wa soka barani Ulaya, iko nyuma kwa pointi saba nyuma ya vinara Man United na
sita, nyuma ya mabingwa watetezi Man
City.
Fergie bosi wa Man United, alisema: “Matokeo ya leo usiku
yanatuweka sisi mbali kidogo na Chelsea
katika mbio za ubingwa wa ligi.
“Sisi bado tuko mbele tukiongoza msimamo wa ligi, lakini Man City
wako karibu yetu na msimu bado ni mrefu.
“Umuhimu wa kushinda bao 1-0 katika baadhi ya mechi,
unawaonesha wapinzani wako kiasi cha ujasiri mlichonacho.
“Kama utaangalia baadhi ya mechi muhimu za matokeo ya bao
1-0 tuliowahi kupata... rejea nyuma kabisa tulipoicaha Newcastle wakati wakiwa pointi tisa juu yetu
mwaka 1996 – ushindi wetu wa 1-0 usiku huo, ukatuwezesha kutupa ubingwa.
“Kulikuwa na umuhimu wa ushindi wa 1-0. tulifanya hivyo kwa
wengi wao.”
No comments:
Post a Comment