Zambia, ambao wanashikilia ubingwa wa Afrika waliotwaa kwenye fainali zilizopita zilizoandaliwa kwa pamoja na Equatoria Guinea na Gabon, watawasili nchini Desemba 18, 2012 na kucheza mechi hiyo ya kirafiki Desemba 22, 2012 kabla ya kurejea kwao Desemba 23, 2012.
“Kwa mara nyingine Tanzania imebahatika kutembelewa na mmoja wa magwiji wa soka barani Afrika baada ya Abeid Pele (wa Ghana) kutembelea nchini mwezi uliopita,” alisema Osiah. “FAZ wametutaarifu kuwa Bwalya ndiye atakayeongoza msafara wa timu itakapokuja nchini na hivyo Watanzania watapata nafasi nyingine ya kukutana na kuongea na mmoja wa magwiji wa Afrika.
“Tuliona jinsi wachezaji wa Serengeti Boys walivyohamasika kutokana na maneno ya Abedi Pele na tunatarajia ndivyo Bwalya atakavyofanya kwa vijana wetu na wadau wa mpira wa miguu. Tutajitahidi kuandaa program itakayowezesha vijana wetu kuongea naye.”
Bwalya alinusurika kwenye ajali hiyo kutokana na kupande ndege tofauti. Hata hivyo, akiwa na kikosi kilichojaa damu Changa, gwiji huyo wa Zambia aliiongoza nchi yake kufika fainali. Kalu aliichezea klabu maarufu ya Uholanzi, PSV Einhoven na baadaye kwenda Mexico ambako alistaafia kabla ya kupewa kazi ya ukocha na baadaye kurejea Zambia ambako pia aliifundisha timu ya taifa.
Chini ya uongozi wake, Zambia imefanikiwa kufuta nuksi ya kukosa vikombe barani Afrika baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mara ya pekee mwaka huu
No comments:
Post a Comment