MANCHESTER, England
GOLI kali la ‘fri-kiki’ kutoka kwa Robin van Persie katika dakika za majeruhi liliwapa Manchester United ushindi wa ugenini wa 3-2 dhidi ya mabingwa Manchester City leo na hivyo kujichimbia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England kwa tofauti ya pointi sita.
Matokeo hayo yalihitimisha takriban rekodi ya miaka miwili ya kutofungwa nyumbani kwa Man City katika Ligi Kuu ya England huku Man U ikiendelea kutesa kileleni kwa kuwa na pointi 39 kutokana na mechi 16, wakati Man City wakibaki katika nafasi ya pili huku wakiwa na pointi 33.
Man United furaha zao zimekatizwa ghafla kwa kitendo cha kumuona mchezaji wao Rio akivuja damu
Pablo Zabaleta akifurahia kurudisha goli na kufanya 2-2
Kikosi cha Man City kilichoanza
Hart, Zabaleta, Kompany, Nastasic, Clichy, Yaya Toure, Barry, Nasri, Silva, Aguero, Balotelli.
Kikosi cha Man United kilichoanza
De Gea, Rafael, Ferdinand, Evans, Evra, Valencia, Cleverley, Carrick, Young, Rooney, Van Persie.
KITENDO CHA RIO KUUMIA:
Rio Ferdinand alipojeruhiwa na kujikuta akivuja damu juu ya jicho lake la kushoto baada ya kupigwa na na kitu kilichorushwa na mashabiki.
Hart akijaribu kumkinga Rio mara baada ya shabiki kuingia uwanjani hapo mwishoni mwa mechi.

wewe ....

Joe Hart kipa wa City akishikana tai na shabiki kumkinga Rio Ferdinand
Shabiki aliyeingia uwanjani akitiwa nguvuni hapa
Tevez hapa alifanya makosa lakini refa akapeta mbele ya Sir Alex Ferguson
Vurugu zikiendelea...
Angalia hii video...
Rio Ferdinand amepatiwa matibabu ya haraka ya kuzuia damu
Ferdinand kisa cha kuumizwa ameshangilia mbele ya mashabiki wa City
Van Persieakishangilia na hapo hapo anamuona Rio akitiririkiwa damu usoni
Ferdinand amerushiwa mashiringi usoni
Ferdinand akiinama kujiuguza na jeraha baada ya mashabiki kurusha coin za pesa
Shabiki likiingia uwanjani na kutaka kukwaruzana na Rio
Joe Hart kipa wa City akishikana tai na shabiki kumkinga Rio Ferdinand
UTATUKOMAA.....
Carlos Tevez akipandishiana na Phil Jones karibu na makocha wote wawili
Mashabiki wa Man City wakiwafanyia vurugu polisi
Rooney pia alirushiwa na mashabiki wa City vitu kama mawe wakati anaenda kupiga kona.
No comments:
Post a Comment