BUKOBA SPORTS

Sunday, December 2, 2012

SIR ALEX FERGUSON ACHUKIZWA NA SAFU YA ULINZI YA TIMU YAKE UNITED!, HUKU MANCHESTER UNITED WAKIINYUKA GOLI 4-3 READING

Sir Alex Ferguson, meneja wa Manchester United, Jumamosi alielezea kwamba hajawahi kuona ulinzi mbovu wa timu yake msimu huu kama alivoshuhudia wakati timu yake ikiwa ugenini Reading, licha ya kuondoka na ushindi wa magoli 4-3 dhidi ya wenyeji.United mara nyingi walionekana dhaifu kutokana na mchezo wa kupanga na kuviziana, na meneja Ferguson alisema ni lazima timu yake kuinua kiwango cha mchezo wao kufikia mwishoni mwa wiki ijayo, wakati watakutana na majirani Manchester City.

"Ulikuwa ni ulinzi mbovu zaidi msimu huu," alielezea Ferguson.
“Lazima tuchukue hatua kuhusu hili”.

"Reading waliweza kuelekeza mipira vyema, lakini kabisa mlikuwa hamna ushindani katika kuzuia hayo."
Mara mbili walilemewa na kuwaacha Reading kutangulia kwa magoli, na hii ikiwa ni mara ya 14 msimu huu kuiacha timu ya upinzani kutangulia kupata bao la kwanza.

Magoli yote saba ya timu zote mbili yalifungwa katika dakika 34 za kipindi cha kwanza katika uwanja huo wa Madejski.
Win: Man UKwa bahati nzuri, Man U waliweza kujibu mashambulizi ya Reading mara mbili, na kuongezea magoli ambayo yaliwawezesha kurudi Old Trafford na ushindi, na wakiwa kileleni mwa ligi ya Premier, sasa tofauti kati yao na wapinzani wao wakuu, majirani Man City, ni pointi tatu.

Man City, wakiwa nyumbani katika uwanja wao wa Etihad, watawakaribisha Man United Jumapili ijayo.
"Tulistahili kutandikwa leo," alisema Ferguson.

"Hakuna aliyefanya juhudi za kushindania migongeo. Pasipo kupendelea, Reading walimiliki mpira vyema, kijana [Nicky] Shorey aliwaelekezea wenzake mipira vyema mno. Tulistahili kufanya vyema zaidi ya hivyo. Tulicheza vibaya mno”, alilalama Ferguson.

"Iwapo utafanya makosa kama hayo katika ulinzi, basi kila wiki kazi yako itakuwa ni juhudi za kuokoa tu. Leo ilikuwa ni juhudi zaidi za kuokoa tu.
"Ilikuwa ni muujiza namna tulivyoshinda kwa ulinzi kama huo. Ninaridhika tu kwa kuwa tuliondoka na ushindi.”

1-0: Reading's Hal Robson-Kanu (centre right) put the home side a goal up after eight minutes
1-0: Reading's Hal Robson-Kanu (centre right) put the home side a goal up after eight minutes

1-1: Anderson equalised for Manchester United shortly afterwards
1-1: Anderson equalised for Manchester United shortly afterwards
1-2: Wayne Rooney found the bottom corner with a penalty to give United the lead after Jonny Evans had been fouled
1-2: Wayne Rooney found the bottom corner with a penalty to give United the lead after Jonny Evans had been fouled

VIKOSI

Reading: Federici, Shorey, Mariappa, Morrison, Cummings, Leigertwood, McAnuff, Tabb, Robson-Kanu (Hunt 83), Le Fondre, Roberts (Pogrebnyak 69)
Subs not used: Taylor, Pearce, Harte, Guthrie, McCleary 
Scorers: Robson-Kanu 8, Le Fondre 19, Morrison 23
Booking: Tabb  
Manchester United: Lindegaard, Rafael (Smalling 31), Evra, Ferdinand, Evans, Anderson (Jones 45), Carrick, Young, Fletcher, Rooney, Van Persie (Welbeck)
Subs not used: De Gea, Giggs, Cleverley, Hernandez
Scorers: Anderson 13, Rooney 16 (pen), 30, Van Persie 34
Booking: Rafael Referee: Mark Halsey
Attendance: 24,095 

2-2: Adam Le Fondre (centre) scores a header to restore parity once again
2-2: Adam Le Fondre (centre) scores a header to restore parity once again
3-2: Reading then took the lead with another header through Sean Morrison
3-2: Reading then took the lead with another header through Sean Morrison

3-3: Wayne Rooney levelled things again with a close-range finish from Patrice Evra's cut back
3-3: Wayne Rooney levelled things again with a close-range finish from Patrice Evra's cut back

3-4: Ten minutes before half-time, Robin Van Persie raced through to score what proved to be the winner
3-4: Ten minutes before half-time, Robin Van Persie raced through to score what proved to be the winner

No comments:

Post a Comment