Nigeria ilipata bao hilo muhimu na la ushindi kupitia kwa msahmbulizi wake Emmanuel Emenike, anayeichezea klabu ya Spartak Moscow ya Urussi kunako dakika ya 23.
Kikosi hicho cha Super Eagles, kilifanya mashambulizi kadhaa katika lango la Burkina Faso, lakini juhudi hizo hazikuzaa matunda.
Baada ya dakika za kwanza 45, zilimalizika huku Nigeria ikiwa kifua mbele kwa bao moja kwa bila.
Awali Nahodha wa Nigeria Joseph Yobo alisema kushinda kombe hilo sio kazi rahisi, ila wamejitolea kucheza kadri ya uwezo wao, kuhakikisha kuwa Nigeria, inaibuka mshindi.
Amesema dhamira yao kuu, ni kufikiria hatua za robo na nusu fainali.
Mcheza kiungo, Victor Moses ambaye anaiakilisha Nigeria kwa mara ya kwanza naye anasema wamejianda vyema na ana matarajio makubwa kuwa watafanya vyema katika mashindano ya mwaka huu.
Nigeria ilipata bao hilo muhimu na la ushindi kupitia kwa msahmbulizi wake Emmanuel Emenike, anayeichezea klabu ya Spartak Moscow ya Urussi kunako dakika ya 23.

Matumaini ya kocha wa Super Eagles, Stephen Keshi, ambaye anaiongoza timu kwa mara ya kwanza katika fainali hizo ya kuandikisha ushindi wake wa kwanza ulitumbukia nyongo pale Burkina Faso iliposawazisha katika dakika za ziada.
Matumaini ya kocha wa Super Eagles, Stephen Keshi, ambaye anaiongoza timu kwa mara ya kwanza katika fainali hizo ya kuandikisha ushindi wake wa kwanza ulitumbukia nyongo pale Burkina Faso iliposawazisha katika dakika za ziada.
Timu zote katika kundi hilo, Ethiopia, Burkina Faso, Nigeria na Zambia sasa zina alama moja kila mmoja.
Nigeria sasa itachuana na Zambia katika mechi yao ijayo kisha icheza na Ethiopia mechi yao ya mwisho ya makundi.
Burkina Faso nayo imeratibiwa kucheza na Ethiopia mechi ijayo kisha ikamilishe kampeinin yake ya raundi ya kwanza na Zambia.
No comments:
Post a Comment