BUKOBA SPORTS

Tuesday, January 22, 2013

MAMIA YA MASHABIKI WA GALATASARAY WAMPOKEA WESLEY SNEIJDER ISTANBUL!

Istanbul
KLABU ya Galatasaray imemnasa kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Uholanzi, Wesley Sneijder kwa ada euro milioni 8.3 kutoka klabu ya Inter Milan ya Italia. Galatasaray yenye maskani yake nchini Uturuki imesema kuwa imesainisha nyota huyo mkataba wenye thamani ya euro milioni kwa mwaka mpaka mwaka 2016 baada ya kushindwa kuafikiana suala la malipo na Inter. Sneijder alijiunga na Inter akitokea Madrid mwaka 2009 na kuisaidia klabu hiyo kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Serie A na Kombe la Italia mwaka 2010. Wakati pazia la usajili wa dirisha dogo likielekea kufungwa Januari 31.
Wananchi wengi wamejitokeza kumpokea kwa wingi kwenye mitaa ya Istanbul na kukutana naye ana kwa ana. Baada ya kuandamwa na wananchi wengi kutokea uwanja wa ndege wa Ataturk airport na huku wakionesha furaha na huku wakionesha kumkubali kiungo huyo mshabuliaji.
Karibu Wesley Sneijder Istanbul
Crowd scene: Sneijder's arrival at Ataturk airport was seen by a host of supporters
Mamia ya watu wakifurika kumuona Sneijder uwanja wa ndege Ataturk
Flare play: There was an air of frenzied excitement in Istanbul at Sneijder's unveiling
washa washa !!
He was mobbed by thousands of fans as he made his way through the streets to talk to the media
Angalia mapaparazi nyuma, wengine kamera, simu na wengine ni furaha tu kumuona live.
 Sneijder met up with officials from Galatasary in the capital
Sneijder akikutana na viongozi mbalimbali hapa
Supporters find every place to shout their approval of Sneijder's signing
Kila mahali ilikuwa ni Sneijder, Sneijder wakilia sahihi yake

No comments:

Post a Comment