Mali ilipata goli la kuongoza katika kipindi cha
kwanza katika dakika ya 21 likifungwa na Mahamadou. Hadi mapumziko Mali
ilikuwa ikiongoza kwa hilo goli.
Kipindi cha pili kilianza kwa Mali tena kufunga katika dakika ya 48, mfungaji akiwa ni Seydou Keita.
Ghana ilijitutumua na kupata bao la kufutia machozi katika kipindi hicho cha pili. Hata hivyo furaha yao haikudumu sana baada ya kuchapwa goli lingine la tatu na la ushindi kwa Mali.
Matokeo haya yanaendeleza ubabe wa Mali dhidi ya
Ghana, ambapo mwaka jana katika mchezo kama huo wa kutafuta mshindi wa
tatu wa michuano ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika 2012, Mali
iliichapa Ghana 2-0.
Ni mwaka mmoja kamili, wakati Ghana na Mali
zilipokuwa zikijiandaa kucheza mechi ya kusaka nafasi ya tatu baada ya
timu zote mbili kupoteza matumaini ya ubingwa zilipotolewa katika nusu
fainali za michuano ya kombe la Afrika za mwaka 2012.
Mchezo huu, unatoa fursa ya kuhitimisha michuano hiyo ambapo bingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2013 atapatikana, ukizikutanisha Nigeria na Burkina Faso hapo keho.
Ghana na Mali baada ya kukosa kombe hili, jitihada zinaelekezwa katika kutafuta nafasi ya kucheza fainali za kombe la dunia za mwaka 2014 zitakazofanyika nchini Brazil.
Seydou Keita akiipatia goli muda mchache baada ya mapumziko dakika ya 48 kipindi cha pili.
Historia imejirudia
Wachezaji wa Mali wakishangilia
Mashabiki wa Mali wakifurahia ushindi wa tatu kwenye uwanja wa Port Elizabeth
Ghana ilijitutumua na kupata bao la kufutia machozi katika kipindi hicho cha pili. Hata hivyo furaha yao haikudumu sana baada ya kuchapwa goli lingine la tatu na la ushindi kwa Mali.
Mchezo huu, unatoa fursa ya kuhitimisha michuano hiyo ambapo bingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2013 atapatikana, ukizikutanisha Nigeria na Burkina Faso hapo keho.
Ghana na Mali baada ya kukosa kombe hili, jitihada zinaelekezwa katika kutafuta nafasi ya kucheza fainali za kombe la dunia za mwaka 2014 zitakazofanyika nchini Brazil.
Wachezaji wa Mali wakishangilia
No comments:
Post a Comment