Manchester United leo wamepanda Pointi 12 mbele juu kileleni mwa Ligi Kuu England baada ya kuifunga Everton Bao 2-0 Uwanjani Old Trafford.
Bao za Kipindi cha Kwanza za Ryan Giggs, akiweka Rekodi ya kuwa Mchezaji pekee kupiga Bao kila Msimu wa Ligi kwa Misimu 23, na lile la Robin van Persie, ndiyo yamewapa ushindi Man United huku wakishuhudiwa na Kocha wa Real Madrid Jose Mourinho ambao watapambana nao Jumatano huko Santiago Bernabeu kwenye Mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.
Baada ya Mechi ya leo, Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, alibainisha kuwa alipanga kubadili Kikosi chake kwa kutumia Wachezaji 7 wengine lakini matokeo ya jana ya kupigwa Man City Bao 3-1 na Southampton yalimfanya abadilike ili awanie kupata pengo la Pointi 12 mbele ya Mahasimu wao Man City.
Ryan Giggs akipongezwa na wenzake baada ya kufunga goli la kwanza na la pekee kupiga Bao kila Msimu wa Ligi kwa Misimu 23

Fellaini akimtoka Tom Cleverley

Ryan Giggs akifunga goli la kwanza

Phil Jones akimkwepa mchezaji wa Everton Pienaar

Robin van Persie akiipatia Manchester United goli la pili na kufanya 2-0 dhidi ya Everton

Van Persie akishangilia baada ya kufunga goli la pili

Antonio Valencia akichuana na Leighton Baines

Phil Jagielka akipiga mpira kulia ni Ryan Giggs

Jonny Evans akikosa kosa goli hapa

Kocha wa United Sir alex Ferguso akitoa maelekezo
VIKOSI:
Man Utd: De Gea, Da Silva, Vidic, Evans (Smalling 81), Evra, Valencia, Cleverley, Jones (Carrick 56), Giggs, Rooney, Van Persie.
Subs not used: Amos, Anderson, Hernandez, Nani, Welbeck.
Goals: Giggs 13, Van Persie 45.
Everton: Howard, Neville, Jagielka, Heitinga, Baines, Mirallas (Naismith 70), Osman, Gibson, Pienaar, Fellaini, Anichebe (Jelavic 57).
Subs not used: Mucha, Oviedo, Hitzlsperger, Stones, Duffy.
Booked: Mirallas, Fellaini
Att: 75,525
Referee: Mark Halsey
No comments:
Post a Comment