BUKOBA SPORTS

Monday, March 18, 2013

CAF: BARRACK YOUNG CONTROLLERS 1 vs AZAM FC 2, AZAM WALETA MATUMAINI BONGO!!

KLABU PEKEE ya Tanzania ambayo bado imo kwenye Michuano ya Klabu Barani Afrika, Azam FC, leo imeanza vyema Mechi yake ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya Kombe la Shirikisho kwa kuifunga Barrack Young Controllers II Bao 2-1 huko Mjini Monrovia, Liberia.
Hadi Mapumziko Azam FC walikuwa nyuma kwa Bao 1-0 lakini Kipindi cha Pili waligangamala na kupiga Bao mbili Wafungaji wakiwa Humphrey Mieno, Mchezaji kutoka Kenya, na Bao la ushindi kupatikana Dakika ya 90 Mfungaji akiwa Seif Abdallah Karihe kufuatia kazi njema ya Khamis Mcha ‘Vialli.’ 
Azam FC na Barrack Young Controllers II watarudiana Jijini Dar es Salaam kwenye Wikiendi ya kuanzia Aprili 6.
Mshindi wa Mechi hiyo atasonga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na watakaofuzu hatua hiyo wataingia hatua ya Makundi itayochezwa Mtindo wa Ligi.
Kufuatia kubwagwa nje ya Michuano ya CAF ya CHAMPIONS LIGI kwa Simba na Jamhuri ya Zanzibar, Azam FC ndie Mwakilishi pekee Barani Afrika.

KIKOSI CHA AZAM FC KILICHOANZA
Mwadini Ally, Himid Mao, Waziri Salum, David Mwantika, Joackins Atudo, Ibrahim Mwaipopo, Humphrey Mieno, Kipre Balou, Khamis Mcha ‘Vialli’, John Bocco, Kipre Tcheche

No comments:

Post a Comment