
Judith amesema hayo muda mfupi uliopita (saa 3:52 asubuhi) wakati akihojiwa katika kipindi cha Super Mix ya East Africa Radio na mtangazaji Zembwela.
Jaydee ameeeleza uamuzi wake wa kutitisha show hiyo kuwa unalenga kutoa nafasi kwa wafiwa wote na wadau wa tansnia ya muziki na wapenzi wa Mangwea kumaliza taratibu za kumsitiri kipenzi chao na kueleza kwamba tarehe nyingine ya shughuli hiyo itatangazwa baadae.
Tangu amekaribishwa studio, Judith Wambura alionekana kuwa na majonzi sana kiasi cha kushindwa kuongea mara kwa mara na kukatisha mazungumzo yake kutokana na kukabwa na kilio.
HII HAPA PICHA YA MWILI WA MAREHEMU ALBERT NGWEA UKIWA MOCHWARI

Tumelazimika kuweka picha hii kutokana na maombi ya mashabiki wake ambao hawatapata nafasi ya kumuaga msanii huyu na kutoa salamu zao za mwisho.....
R.I.P NGWEA
No comments:
Post a Comment