BUKOBA SPORTS

Thursday, July 11, 2013

KOMBE LA DUNIA U-20: FRANCE 2 vs GHANA 1, GHANA WATEMWA NJE KUGOMBEA NAFASI YA TATU, MUUAJI AKIWA FLORIAN THAUVIN, FAINALI NI FAINALI FRANCE v URUGUAY!

BURSA, TURKEY - JULY 10: Florian Thauvin of France scores his goal during the FIFA U-20 World Cup Semi-Final match between France and Ghana at the Ataturk Stadium on July 10, 2013 in Bursa, Turkey. (Photo by Jamie McDonald - FIFA/FIFA via Getty Images)
2013_FIFA_U-20_World_Cup_logo (1)MSHINDI WA 3: GHANA v IRAQ!!
GHANA, Wawakilishi pekee wa Afrika waliobakia GHANA, Jana Usiku walitupwa nje ya MASHINDANO Ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Vijana chini ya Miaka 20, U-20, walipotolewa kwenye Nusu Fainali iliyochezwa huko Nchini Turkey kwa kufungwa Bao 2-1na France.

France sasa itacheza Fainali na Uruguay ambayo iliitoa Iraq kwa Penati 7-6 baada ya kutoka Sare ya Bao 1-1 katika Nusu Fainali nyingine iliyochezwa huko Turkey hiyo Jana kwenye Mechi iliyomalizika 1-1 katika Dakika 90 na kubaki 1-1 hadi Dakika 120 zilipomalizika na ndipo Tombola ya Mikwaju ya Penati kuipa ushindi Uruguay.

FRANCE 2 vs GHANA

Huko Bursa Ataturk Stadyumu, Mjini Bursa, Jana France ilitinga Fainali kwa kuilaza Ghana Bao 2-1 na hii ni mara ya pili kwa France na Ghana kukutana kwenye Mashindano haya huko Turkey.
Awali, kwenye Mechi ya Kundi lao, France iliipiga Ghana Bao 3-1.
Kwenye Nusu Fainali ya Jana, France walitangulia kufunga kwa Bao la Thauvin lakini Dakika 4 baadae Mfungaji hatari wa Ghana, Assifuah, alisawazisha.

Hadi Mapumziko, Bao zilikuwa 1-1.
Kipindi cha Pili, Dakika ya 74, Thauvin tena akaifungia France Bao la Pili na la ushindi
.

No comments:

Post a Comment