BUKOBA SPORTS

Thursday, July 11, 2013

LIVE MATCH: KAGASHEKI CUP 2013, MIEMBENI 2 vs RWAMISHENYE 2, MECHI IKIISHA KWA MASWALI MENGI NA UTATA!!!

Wachezaji na waamuzi wakiingia uwanjani
Timu zikisalimiana muda mfupi kabla ya kuanza
Picha ya pamoja na timu kapteni na refa

Wachezaji wa Rwamishenye wakiomba kushinda hapa!
Kikosi cha Rwamishenye kilichoanza
Kikosi cha Miembeni kilichoanza
Mashabiki wa Miembeni



wadau wakifatilia kabumbu kwa hali ya juu sana na makini
Wadau jukwaani wakifatilia soka uwanja wa Kaitaba
Bao!!! la...laa!!!
Miembeni wakishangilia kwa furaha baada ya kupata bao la frii kiki kuelekea golini
Raha ya kupata bao
Wachezaji wa Miembeni wakipongezana baada ya kufunga goli la kwa kwanza na kufanya 1-0 dhidi ya rwamishenye

Wachezaji wa Miembeni wakishangilia kwa kurudi kati

Wakati mtananange unaendelea kwenye jukwaa la Balimi palikuwa hapatoshi mashabiki baadhi walikuwa wanatupiana makonde
Kipa wa Miembeni akitoa kwa kupangua mkwaju wa penati uliopigwa na mchezaji wa Rwamishenye

Patashika za hapa na pale kwenye jukwaa la Balimi!!!!!!!!!

Wachezaji wa Miembeni wakishangilia baada ya kutupia nyavuni na kufanya 2-0

Miembeni wakishangilia wachezaji

Rwamishenye nao wakafunga bao na kufanya 2-1 kipindi cha pili

...Zamu yetu sasa na sisi tushangilie!!


Baadaye kidogo Rwamishenye wakafunga bao la kusawazisha la utata na kufanya 2-2

Wakati kocha anapuliza kipenga cha kumaliza mechi, Wachezaji wa  timu ya Rwamishenye walifunga bao jingine la utata tena na kumfanya refa ababaike tena huku wachezaji wakimlalamikia kuwa bao la haki!!!

Refa alimaliza mechi kama hivi na huku lawama zikimwandama hadi nje ya uwanja !!

Mashabiki wakiandamana nje ya uwanja kujua kuwa lipi na lipi ni 2-2 au ni 3-2, swali hili lilipata msemaji wake ambaye ni Refali wa mchezo huo kwa kudai kuwa mtanange huu ni sare ya 2-2.

Mashabiki wakijiuliza yaliyotokea uwanjani jioni hii kati ya Miembeni na Rwamishenye

Siyo kweli!!! ongea ukweli ....hapa kuna namna!!! ni Kamala akiteta na kiongozi mmoja ambaye jina lake halikupatikana mara moja!

No comments:

Post a Comment