David Moyes amethibitisha kuwa Robin van
Persie hakuumia sana kiasi cha kumfanya aikose pia Mechi ya Manchester
United ya Jumatano na Liverpool Uwanjani Old Trafford ambayo ni ya
Raundi ya Tatu ya Capital One Cup.
Jumapili, Van Persie hakucheza kwenye Mechi ya Ligi Kuu England huko Etihad walipofungwa 4-1 na Man City.
Moyes alisema: “Tunafikiri yuko sawa. Tutampa kila nafasi. Hakuumia sana.”
Moyes alibainisha kuwa Staa huyo alikuwa
akisikia maumivu kidogo kwenye Nyonga na ili kumlinda asijiumize zaidi
waliamua kumpumzisha kwenye Mechi na Man City.
No comments:
Post a Comment