BUKOBA SPORTS

Tuesday, December 17, 2013

GLENN HODDLE NJIANI KUTUA TOTTENHAM KUINOA TIMU HIYO BAADA YA ANDRE VILLAS BOAS KUFUKUZWA JANA ASUBUHI.

Huenda meneja wa zamani wa Tottenham Hotspurs, Glenn Hoddle akarejea tena katika klabu hio kuziba pengo lililoachwa na kocha Andre Villa-Boas ambaye hapo jana alitimuliwa.

Boas alitimuliwa baada ya timu ya Tottehnam kuchapwa na Liverpool mabao 5-0.Glenn Hoddle aliyeinoa Spurs kati ya mwaka 2001 na 2003, anatajwa kua miongoni mwa makocha ambao huenda wakaziba pengo hilo, na pia yupo karibu sana na mwenyekiti wa Spurs, Daniel Levy. 
Kocha wa zamani wa Uingereza Fabio Capello, Meneja wa Swansea Michae Laudrup na mkurugenzi wa ufundi wa Tottehnam Franco Baldini, ni baadhi ya wengine wanaotajwa kua huenda wakachukua na fasi hio. 
Wakati Tottenham wakitimua kocha kwa upande wake Meneja wa Liverpool Brenden Rodgers amesema hatua ya timu yake kuisambaratisha Tottenham kwa magoli 5 - 0 katika uwanja wao wa nyumbani wa White Hart Lane ni moja kati ya mechi ya viwango vya juu vilivyoonyeshwa na Liverpool katika kipindi cha uongozi wake.AVB alifukuzwa siku moja baada ya kipigo cha bao 5-0 kutoka kwa majogoo Liverpool.Rodgers alishika hatamu ya kuinoa Liverpool mwaka 2012 ambapo kwa sasa timu hiyo ipo nafasi ya pili ikiwa nyuma ya Arsenal katika msimamo wa ligi kuu ya England.

No comments:

Post a Comment