BUKOBA SPORTS

Wednesday, February 5, 2014

COPA DEL REY: REAL MADRID 3 v ATLETICO MADRID 0, REAL WAFANYA KWELI ....JESE RODRIGUEZ AFUNGA BAO MOJA..RONALDO AKIONGOZA MASHAMBULIZI.

Nusu Fainali za Kombe la Mfalme huko Spain, Copa del Rey, kuanza usiku huu  Jumatano, Mtanange unaotangulia ni wa Mechi ya kwanza utakaochezwa El Estadio Santiago Bernabeu ambapo Wenyeji Real Madrid watawakaribisha Mabingwa Watetezi wa Kombe hili, ambao pia ni Vinara wa La Liga, Atletico Madrid, ambao pia ni Mahasimu wao wakubwa....
Pepe leads the celebrations after his shot deflected off Emiliano Insua to give Madrid the lead against Atletico.
Kipindi cha kwanza dakika ya 17 Atletico Madrid wamejifunga bao kupitia kwa mchezaji wao Emiliano Insua na kufanya Real waitangulie kwa bao hilo kipindi cha kwanza kwa kumalizika kwa bao 1-0, Kipindi cha pili dakika ya 57 Jese Rodriguez amewapatia bao la pili na kufanya 2-0 Atletico Madrid.Jese celebrates after putting Real two goals to the good against Atletico.
Jese Rodriguez akishangilia bao lake dakika ya 57 kipindi cha pili.
Wachezaji wa Real Madrid wakishangilia bao lao la kwanza

Cristiano Ronaldo akijaribu kumtoka mchezaji wa Atletico de Madrid usiku huu

Dakika ya 73 kipindi cha pili Atletico Madrid wakajifunga tena bao safi kwa kupitia mchezaji Miranda. Bao hilo la kujifunga kwa Miranda limehitimisha jumla ya bao 3-0 na mpira kumalizika huku kocha wao Atletico Madrid Diego Simeone akipewa kadi ya njano. 

Zinedine Zidane nae alikuwemo uwanjani kuwacheki Real MadridFuming: Atletico boss Diego Simeone has words with the fourth official during the game
Kocha Diego Simeone amepewa kadi ya njano kwenye mtanange huu.

COPA del REY
NUSU FAINALI
Marudiano

Jumanne Februari 11
23:00 Atletico de Madrid v Real Madrid CF [Estadio Vicente Calderon]
Jumatano Februari 12
24:00 Real Sociedad v FC Barcelona [Estadio Anoeta]
FAINALI
Aprili 19

No comments:

Post a Comment