Familia ya aliyekuwa staa wa filamu za Fast & Furious, Paul Walker(40) huenda ikaingia kwenye mgogoro kufuatia urithi alioacha mcheza filamu huyo kuhusiana na mtu anayetakiwa kurithi mali zake. Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ uliweza kuzinyaka dokumenti hizo za urithi na kuziweka wazi bila chenga.
Muigizaji huyo aliyekuwa na utajiri unaokadiriwa kufikia dola za kimarekani milioni 25(Tsh 40 Bilioni) alitanabaisha ya kwamba endapo ikatokea akafariki kiasi hicho chote cha utajiri wake apewe mtoto wake wa kike anayeitwa ‘Meadow’ ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 15 .
Bado haijaweza kufahamika wazi kama mama mzazi wa Meadow anayeitwa Rebecca Soteros ambaye kwa sasa anaishi na mtoto wake huyo kama atakubaliana na shauri lililotolewa na baba mkwe wake.
Kipindi cha nyuma marehemu Walker aliwahi kunukuliwa akisema ya kwamba angependa kuona mama yake mzazi anakuwa msimamizi wa mali za mtoto wake endapo ikatokea akarest in Peace. Nyota ya staa huyo ilizimika ghafla kama mshumaha baada ya kupata ajali mbaya ya gari iliyochukua maisha yake na rafiki yake Roger Rodes February 30 mwaka jana.
No comments:
Post a Comment