BUKOBA SPORTS

Thursday, February 27, 2014

VERONICA CAMPBELL-BROWN KUSHIRIKI RIADHA MWAKA HUU

Veronica Campbell-Brown atashiriki mashindano ya riadha mwaka huu .
Campbell ambaye ni mshindi mara mbili wa Olimpiki katika mbio za mita 200 alishinda rufaa aliyowakilisha katika mahakama kuu ya Rufaa katika michezo Duniani CAS.

Shirikisho la riadha la Jamaica lilimpiga marufuku mwanariadha huyo lilipompata na hatia ya kutumia dawa zilizoharamishwa za kutumua misuli katika mashindano ya kitaifa mwezi Mei.
Campebell ambaye amekuwa akisisitiza kuwa hakuwahi tumia dawa hiyo iliyopigwa marufuku na anasema alifedheheshwa sana na matukio yaliyomnyima fursa ya Kutetea taji lake la mita mia mbili la dunia mwaka uliopita .
Campbell anatarajiwa kuiwakilisha Jamaica katika mashindano ya ndani yatakayoandaliwa huko Poland mwezi ujao na Labda mashindano ya Jumuiya ya Madola yatakayofanyika mwezi Julai .

No comments:

Post a Comment