BUKOBA SPORTS

Sunday, March 9, 2014

FA CUP: HULL CITY 3 v SUNDERLAND 0, DAVIES, MEYLER NA MATTY FRYATT WAIPATIA USHINDI HULL CITY


Timu ya Sunderland leo imekubali kipigo cha bao 3-0 kutoka kwa timu ya Hull City iliyokuwa inachezea kwao kwenye uwanja wa KC ikiongozwa na mwamuzi C. Pawson mbele ya Mashabiki 20,047.

Bao za Hull City zimefungwa zote kipindi cha pili, Bao la kwanza likifungwa na Curtis Davies katika dakika ya 68, bao la pili katika dakika ya 72 likifungwa na David Meyler. Dakika chache baadae kwenye dakika ya 77 Hull waliongeza bao jingine kupitia mchezaji wao Matty Fryatt. Hii ni mara ya kwanza kwa Hull City, ambao wako chini ya Steve Bruce, Mchezaji wa zamani wa Man United, kutinga Nusu Fainali ya FA CUP katika Miaka 84.
Wachezaji wa Hull City wakishangilia mara baada ya kuifunga SunderlandKwenye patashika...
    ROBO FAINALI
Jumamosi Machi 8
Arsenal 4 v Everton 0
Jumapili Machi 9
Sheffield United 2 v Charlton 0
Hull City 3 v Sunderland 0
Manchester City 0 v Wigan 0*

NUSU FAINALI: Jumamosi Aprili 12 & Jumapili Aprili 13
FAINALI: Jumamosi Mei 17

No comments:

Post a Comment