Mchakato wa Wasanii wa Maigizo Bukoba unaendelea kushika kazi katika Mji wa Bukoba. Wasanii wakiendelea kuoneshana ubabe wa Kuigiza na hatimae kumpata mmoja Mkali ziadi. Jumapili 9, March 2014 Ulifanyika Mchujo wa kuwapata wasanii wa kusonga mbele kwa wale walifanya Vizuri na wengine walipunguzwa na Majaji katika Ufukwe wa Ziwa Victoria pande za Kiroyera Beach. Majaji wote wanafanya kazi zao vyema na wamesisita kuwa hakuna upendeleo wowote ule ni kujituma na kuonesha Kile kinachoelimisha na kuwafunza Wananchi na Jamii kujumla. Na Hatimae kumpata mkali wa wote.
Msanii wa Maigizo Bukoba Teso Boy akionesha kipaji chake mbele ya Umati wa Watu wengi walikujitokeza kwa wingi katika ufukwe wa Ziwa Victoria pande za Kiroyera Beach.
Wadau wa Maigizo Bukoba wakiwacheki wenzao Uwanjani
Jaji Bi. Merina N. Katambe akitoa neno
Huyu nae...Mganga wa Kienyeji...
Kuigiza si kazi ndogo!!! Jamii lazima uioneshe kile wanachojielimisha!!!
Kuigiza siyo mchezo.....Mvuvi kaibiwa pochi yake ...nini kinafata baada ya kumpata kibaka!!
No comments:
Post a Comment