BUKOBA SPORTS

Tuesday, May 13, 2014

TIM SHERWOOD ATIMULIWA UMENEJA TOTTENHAM, NI BAADA YA MIEZI 6 TUU!!

Sixth: Sherwood's last game was a 3-0 win over Aston Villa, which secured Spurs Europa League football Tottenham imemtimua Meneja wao Tim Sherwood licha ya Klabu hiyo kumaliza Nafasi ya 6 kwenye Ligi Kuu England na kupata nafasi kucheza EUROPA LIGI Msimu ujao.
Sherwood, Miaka 45, alitwaa wadhifa wa Umeneja Mwezi Desemba Mwaka Jana baada kufukuzwa kazi Andre Villas-Boas na yeye kusaini Mkataba hadi mwishoni mwa Msimu wa 2014/15.
Wakitangaza uamuzi huu, Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy, amenukuliwa akisema: “Tulikubaliana Mkataba wa Miezi 18 na kilikuwapo Kipingele cha kuuvunja mwishoni mwa Msimu huu na sisi tumekitumia.” 
Inaaminika hivi sasa Tottenham inao walengwa wawili, mmoja akiwa Meneja wa Southampton, Mauricio Pochettino, na Bosi wa Ajax, Frank de Boer.

No comments:

Post a Comment