BUKOBA SPORTS

Monday, August 25, 2014

ETIHAD...MANCHESTER CITY vs LIVERPOOL

MABINGWA wa England, Manchester City, chini ya Meneja wao Manuel Pellegrini, Leo Jumatatu Usiku wanaingia Uwanjani kwao Etihad kuivaa Liverpool, Timu ambayo Msimu uliopita ilimaliza Nafasi ya Pili.Running machine: Right back Pablo Zabaleta is one of City's more consistent performers 
Hii ni Mechi ya pili kwa kila Timu kwenye Msimu mpya wa Ligi Kuu England baada ya Wikiendi iliyopita zote kushinda Mechi zao za kwanza.
Man City walianza Ugenini huko St James Park na kuifunga Newcastle Bao 2-0 na Liverpool kuanza kwao Anfield na kushinda kwa mbinde Bao 2-1 walipoifunga Southampton huku Bao la ushindi likifungwa mwishoni na Daniel Sturridge.
Hotshot: Daniel Sturridge is taking on the mantle of Liverpool's main man after Luis Suarez's departure 
Wakati Liverpool wametumia zaidi ya Pauni Milioni 100 kuimarisha Kikosi chao kwa Wachezaji wengi wapya, Man City wao Kikosi chao kwa ujumla ni kile kile cha Msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment