BUKOBA SPORTS

Monday, September 29, 2014

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: JUMANNE MANCHESTER CITY vs AS ROMA. HAPATOSHI LEO ETIHAD!!

Mabingwa wa England, Manchester City, baada ya kuchapwa Mechi yao ya kwanza ya Kundi E la UEFA CHAMPIONS LIGI na Bayern Munich, Jumanne Usiku wako kwao kucheza Mechi yao ya pili na AS Roma ambayo ilishinda Mechi yake ya kwanza.
City wanatarajiwa kumrejesha langoni Kipa wao Joe Hart baada ya Meneja Manuel Pellegrini kumpiga Benchi Mechi mbili Wiki iliyopita ile ya Capital One Cup walipoibamiza Sheffield Wednesday Bao 7-0 na Jumamosi kwenye Ligi walipoichapa Hull City 4-2.
Kwenye Mechi ya kwanza ya Kundi lao, Man City walichapwa Bao 1-0 na Bayern Munich huko Germany na AS Roma kuibamiza CSKA Moscow Bao 5-1 huko Italy.
Akikiri umuhimu wa Mechi hii, Pellegrini amesisitiza ushindi kwa Mechi yao hii ya Nyumbani lakini wana kibarua kigumu kwani AS Roma hivi sasa inawika na wako kileleni Serie A pamoja na Mabingwa Juventus baada wote kushinda Mechi zao 5 zote za mwanzo.
Pia, AS Roma huenda wakamchezesha Fulbeki wa zamani wa Chelsea, Ashley Cole, ambae sasa yuko na Klabu hiyo.
Cole has failed to replicate the high standards he had previously shown in the Premier LeagueAshley Cole kurudi England kukwaana kwenye Uefa na wachezaji wa Man City.

No comments:

Post a Comment