BUKOBA SPORTS

Saturday, October 25, 2014

EL CLASICO - REAL MADRID v BARCELONA: JE RONALDO ATAWEZA KUMFUNGA KIPA CLAUDIO BRAVO LEO?? REFA NI G. MANZANO

LEO JUMAMOSI ndio Siku ambayo Vigogo wa Soka huko Spain, Real Madrid na FC Barcelona, watakapocheza Mechi yao ya kwanza ya La Liga Msimu huu Uwanjani Santiago Bernabeu kwenye pambano ambalo hubatizwa Jina rasmi ‘El Clasico.’
Msimu huu, Cristiano Ronaldo ameshapiga Bao 15 katika Mechi 7 za La Liga na anakutana na Kipa wa Barcelona Claudio Bravo ambae hajafungwa hata Bao 1 katika Mechi 7 za La Liga.

LUIS SUAREZ: KUCHEZA!
Meneja wa Barcelona, Luis Enrique, ametoboa kuwa Luis Suarez atacheza Mechi yake ya kwanza ya La Liga baada ya kumaliza Kifungo chake cha Miezi Minne lakini Meneja huyo amekataa kusema kama Straika huyo wa Urguay ataanza Mechi hiyo.El Clasico: Barcelona new boy Luis Suarez to add bite to biggest game in footballNeymar na Suarez
VIKOSI VINAWEZA KUWA HIVI:
11 WA KUANZA.
Real Madrid (Possible, 4-4-2): Casillas; Carvajal, Sergio Ramos, Pepe, Marcelo; Isco, Kroos, Modric, Rodriguez; Ronaldo, Benzema.
Out: Bale (groin).

Barcelona (Possible, 4-3-3): Claudio Bravo; Alves, Mathieu, Pique, Alba; Mascherano, Xavi, Iniesta; Neymar, Messi, Suarez.
Referee: G Manzano 


LA LIGA:RATIBA
Jumamosi Oktoba 25
17:00 UD Almeria v Athletic de Bilbao
19:00 Real Madrid CF v FC Barcelona
21:00 Valencia v Elche CF
23:00 SD Eibar v Granada CF
23:00 Cordoba v Real Sociedad
Jumapili Oktoba 26
14:00 Malaga CF v Rayo Vallecano
19:00 RCD Espanyol v Deportivo La Coruna
21:00 Sevilla FC v Villarreal CF
23:00 Getafe CF v Atletico de Madrid

No comments:

Post a Comment