Gonjwa la Ebola limeikumba Afrika Magharibi na kuua Watu zaidi ya 4,000 na hivi sawa huko Uingereza Vituo vya Forodha vya Majini na kwenye Ndege Watu hupimwa Ugonjwa huo.
Sasa Klabu ya Newcastle nayo imeamua kuwapima Wachezaji wao Waafrika wanaorejea Klabuni baada ya kucheza Mechi za Kimataifa na Nchi zao.
Wachezaji wa Newcastle, Papiss Cisse, anaetoka Senegal, na Cheik Tiote, wa Ivory Coast, walikwenda Nchini mwao na pia kusafiri na Timu zao kucheza Mechi za Makundi za AFCON 2015 huko Tunisia na Congo DR.
Meneja wa Newcastle, Alan Pardew, amekiri Klabu yao watakuwa wapuuzi ikiwa hawaukubali Ugonjwa huo.
Pardew ameongea: “Tunao mkakati wakirudi wao na Familia zao wataangaliwa. Hii ni kuwalinda na kuwasaidia.”
Nchi 3 tayari zilishapigwa marufuku na CAF kucheza Mechi kwao baada ya kuvamiwa na Ugonjwa huu na hizo ni Liberia, Guinea na Sierra Leone
No comments:
Post a Comment