BUKOBA SPORTS

Friday, October 3, 2014

MESSI KUTINGA MAHAKAMANI BAADA YA RUFAA YAKE KUKATALIWA!

LIONEL MESSI atalazimika kwenda Mahakamani kujibu Kesi inayomkabili ya ukwepaji Kodi baada ya Rufaa yake kupinga kuhusishwa na Kesi hiyo kutupwa na Jaji huko Barcelona.
Messi, pamoja na Baba yake Mzazi, Jorge Messi, ambae ndie Wakala wa Mchezaji huyo anaesimamia masuala yake yote ya Kifedha, wanakabiliwa na Mashitaka ya kukwepa kulipa Kodi na kuisababisha Nchi hasara ya Euro Milioni 4 kwenye Kipindi cha kati ya Mwaka 2007-09.
Hata hivyo, Messi na Baba yake wamekana Mashitaka hayo ambayo yanadai walitumia Kampuni huko Belize na Uruguay kuuza Haki za Picha na Matangazo ya Staa huyo ikiwa ni njia ya kukwepa kulipa Kodi huko Spain.
Alipowasilisha Rufaa yake, Messi alijitetea kuwa hajui masuala ya Fedha lakini Jaji huyo alitupilia mbali utetezi huo na kutaka aburuzwe Mahakamani kujibu Kesi yake.

Mwezi Agosti, Jorge Messi alilipa Euro Milioni 5 kwa Wakusanya Kodi huko Spain ikiwa ni Kodi inayodaiwa kukwepwa kulipwa pamoja na riba yake.
Mshahara anaolipwa Messi na Barcelona ni Euro Milioni 16 kwa Mwaka na pia huvuna Mapato mengine mengi kutoka kwa Wadhamini Dunia nzima.

No comments:

Post a Comment