BUKOBA SPORTS

Saturday, January 31, 2015

FULL TIME: REAL MADRID 4 vs 1 REAL SOCIEDAD, KARIM BENZEMA, JAMES NA RAMOS WAIPA USHINDI REAL BILA STAA WAO RONALDO!!

Karim akishangilia bao lake la pili

Sergio Ramos akipeta baada ya kuifungia bao Real Madrid leo huku wakicheza bila Staa wao Cristiano Ronaldo.

Hatari tupu!!

James Rodriguez alisawazisha bao mapema dakika ya tatu

1-1

Karim Benzema akifanya yake leo

Real Sociedad ndio walianza kupata bao mapeema dakika ya 1 kupitia kwa Aritz Elustondo nao Real Madrid walisawazisha kupitia kwa James Rodríguez dakika ya 3 na kuwa 1-1.
Sergio Ramos dakika ya 37 anaipachikia bao la pili Real Madrid na kufanya 2-1 dhidi ya Real Sociedad.

Dakika ya 52 Karim Benzema aliwachapa bao la tatu Real Sociedad na kufanya Timu yake Real kuwa mbele ya bao 3-1 baada ya kupata ushirikiano safi kutoka kwa Gareth Bale. 

Bao la 4 na la mwisho lilifungwa na Karim Benzema dakika 76.Wachezaji wa Real Sociedad wakipongezana baada ya kupata bao wakiwa wa kwanza..Mpaka dakika 90 zinamalizika 4-1 na hivi ndivyo Kocha Moyes anavyoonekana..

No comments:

Post a Comment