BUKOBA SPORTS

Sunday, February 15, 2015

BARNABA BOY NA AMINI WAWASHA MOTO VALENTINE DAY BUKOBA. WAPENDANAO WASHEREHEKEA SIKU YAO MAALUM NDANI LINA'S NIGHT CLUB.

Amini na Barnaba wakiwasha Moto kwa nyimbo murua za Mapenzi siku ya Valentine day 14.02.2015 kwenye Ukumbi wa Lina's Bukoba Usiku huu.
Msanii wa Muziki wa Bongo flava Barnaba akiimba


Siku ya wapendanao ni sikukuu ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 14 Februari ya kila mwaka (Valentine Day). Historia yake imeanzia karne ya 3 huko Roma ambapo alikuwapo padri Valentinus ambaye akaja kuheshimiwa kama mtakatifu hasa tarehe hiyo.Keki ya Valentine day.
Inasemekana kwamba Kaisari wakati huo alikuwa Claudius II: yeye aliona kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule asiyeoa wala kuwa na familia (kapera). Hivyo alipiga marufuku ndoa kwa askari.
Valentinus alipinga jambo hili hivyo kuendelea kufungisha ndoa kwa siri. Mfalme Claudius alipopata habari hizi aliamuru Valentinus akamatwe na kuuawa.
Kuna hadithi nyingine ya kuwa akiwa gerezani Valentinus aliandika barua ambayo ilikuwa na salamu za kwanza za Valentine kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani; mwisho wa barua alihitimisha kwa maneno haya: Kutoka kwa Valentinus wako.
Toka hapo Valentine anakumbukwa kama mtetezi wa wapendanao na sikukuu yake kuadhimishwa kote duniani.Msanii Barnaba akiimba kwa hisia moja ya Wimbo wake kwenye Usiku wa Maalum wa Mahusiano siku ya 'Valentane Day' ambao Umeandaliwa na Zachwa Investment wakishirikiana na Shemeji Investment usiku huu kwenye Ukumbi wa Lina's Night Club.

Deo akiteta jambo na Mzee wa Leo leo..

Hii ndio Maana inaitwa Valentine Day...yaani Siku ya Wapendanao,...cheki furaha zao!!

Barnaba na Amini wakiporomosha burudani ya nguvu na ya aina yake kwa mashabiki wao ndani ya Ukumbi wa Lina's Night Club Mjini Bukoba Usiku huu huku Mashabiki wakipata fursa ya kuchagua nyimbo wazipendazo zinazoendana na usiku huu wa Wapendanao.
Wapendanao
Barnaba akiwajibika kutoa Burudani kwendana na Siku hii ya Wapendanao(Valentine Day).

Bi. Regina
BONYEZA HAPA CHINI KUENDELEA NA MATUKIO ZAIDI...







Ras Nod(katikati) akiwa na Mzee wa Robo saa na Barnaba katika Usiku wa Wapendanao katika Ukumbi wa Lina's Night Club.









Mr na Mrs Gabriel Mageni walipata zawadi baada ya kutokelezea “couples”
Picha ya Pamoja ilipigwa..
“couples” iliyonoga na kutokelezea ilipata Zawadi nono.




Wadau









Amini

No comments:

Post a Comment