BUKOBA SPORTS

Thursday, February 12, 2015

COPA DEL REY: BARCELONA 3 vs 1 VILLAREAL

Barcelona wameanza vyema Nusu Fainali ya Copa del Rey walipoichapa Villareal 3-1 Uwanjani Nou Camp katika Mechi ya Kwanza na Timu hizi zitarudiana Nyumbani kwa Villareal Machi 4.
Hadi Mapumziko Barcelona walikuwa mbele kwa Bao 1-0 ambalo alifunga Lionel Messi katika Dakika ya 41.
Dakika ya 48 Manu Trigueros aliisawazishia Villareal lakini Dakika 1 baadae Andres Iniesta aliwapa Barca Bao la Pili.
Barca walifunga Bao la 3 Dakika ya 63 kupitia Gerard Pique aliefunga kwa Kichwa kufuatia Kona ya Messi.
Dakika ya 70 Barca walipewa Penati ambayo ilipigwa na Neymar na Kipa Asenjo kuokoa.
Hatari tupu!! Kocha wa Barca nae Furaha tupu!

No comments:

Post a Comment