FA CUP: DROO ROBO FAINALI KUFANYIKA LEO KABLA YA MECHI YA PRESTON NORTH END vs MANCHESTER UNITED
Usiku huu ni wenyeji Preston North End vs Manchester United, Nani kuibuka kidedea na kutinga Robo Fainali!Mechi hiyo mwisho ya Raundi ya tano itachezwa leo hii Jumatatu Februari 16 usiku saa nne na dakika 45 kwa saa zetu za Afrika Mashariki (22:45) kati ya wenyeji Preston North End vs Manchester United huko Deepdale, Wenyeji Preston North End, Timu ya Daraja la chini Ligi 1, watacheza na miamba ya Soka ya England Manchester United katika Mechi ya mwisho ya Raundi ya 5 ya FA CUP kuwania nafasi moja iliyobaki kutinga Robo Fainali.Preston North End wanaongozwa na Simon Grayson ambae Mwaka 2010 aliiongoza Leeds United kuibwaga Man United nje ya FA CUP kwa Bao 1-0 Uwanjani Old Trafford kwa Bao la Jermaine Beckford ambae sasa ni Mchezaji wa Preston lakini ataikosa Mechi hii kwa kuwa ni mgonjwa. Lakini Preston wanaweza kumtumia Mkongwe wa Miaka 38, Kevin Davies, ambae ni Straika wa zamani wa Bolton Wanderers mwenye Rekodi ya kuwa na Kadi nyingi katika Historia ya Ligi Kuu England ambae ana Historia ndefu ya kukwaruzana na Man United kila wanapokutana. Mwaka 2007 huko Reebok Stadium Davies alimchezea Rafu mbaya Patrice Evra kiasi cha Sir Alex Ferguson kupandwa jazba kwenye Benchi na hasira hizo zilipozwa na Refa Mark Clattenburg kumpa Kadi Nyekundu Davies. Inadaiwa baada ya tukio hilo Evra alimuuliza Davies kwanini Siku zote wakikutana humuumiza na Davies kujibu: “Kwa sababu sikupendi!”
No comments:
Post a Comment