BUKOBA SPORTS

Saturday, February 14, 2015

REAL MADRID 2 - 0 DEPORTIVO LA CORUNA, ISCO NA BENZEMA WAIPAISHA TENA KELELENI REAL POINTI 4!

Isco na Karim Benzema leo hii waipa Ushindi timu yao Real Madrid ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Deportivo La Coruna kwenye Uwanja wao wa Nyumbani kwao Santiago Bernabeu waliongeza pengo la uongozi wao na kuwa Pointi 4 mbele ya Timu ya Pili Barcelona baada ya kuwafunga Deportivo La Coruna Bao 2-0.
Hadi Mapumziko Real waliongoza kwa Bao la Dakika ya 22 la Isco aliefunga baada ya Krosi ya Garreth Bale kumkuta Karim Benzema alieisindikiza Golini na Ronaldo kushindwa kuunganisha na Mpira kumkuta pembeni Arbeloa ambae aliurudisha nyuma na Isco kuachia Shuti lililotinga Wavuni.
Bao la Pili la Real lilifungwa Dakika ya 73 na Karim Benzema.
Nyota wa Real, Ronaldo na Garreth Bale, walikosa Mabao wakati Mashuti yao mawili yalipopiga Posti.
Hii Leo Barcelona watakuwa Nyumbani Nou Camp kucheza na Levante na Mabingwa Watetezi Atletico Madrid, ambao wako Pointi 7 nyuma ya Real, wako Ugenini kucheza na Celta Vigo.
Ronaldo akipanga kumchomoka Mchezaji wa Deportivo La Coruna kwenye Uwanja wa BernabeuTaswira.

No comments:

Post a Comment