Rodgers amekiri kuwa Wachezaji Vijana Siku zote hufanya makosa lakini kikubwa ni kujifunza toka makosa hayo.
Hata hivyo Rodgers amesisitiza kuwa Adhabu yeyote itakayotolewa itakuwa ni kitu cha ndani ya Klabu.
Hivi sasa Sterling na Liverpool ziko kwenye mvutano baada ya Staa huyo kugomea kusaini Mkataba mpya huku kukiwa na tetesi yuko mbioni kuhamia Klabu kubwa Ulaya huku Real Madrid, Barcelona, Chelsea na Arsenal zikitajwa kuwa zinamlenga.
Baada ya kuibuka tetesi hizo Liverpool ilidai Sterling haendi popote na kusema mazungumzo ya Mkataba mpya yataendelea mwishoni mwa Msimu.
No comments:
Post a Comment