BUKOBA SPORTS

Saturday, April 25, 2015

LOUIS VAN GAAL: 'RYAN GIGGS ATANIRITHI MIMI MAN UNITED!'

Meneja wa Manchester United Louis van Gaal anaamini kuwa Klabu hiyo itamteua Ryan Giggs kama mrithi wake.
Msimu uliopita, Giggs aliiongoza Man United kwa Mechi 4 baada ya kutimuliwa David Moyes na Mwezi Mei akateuliwa kuwa Meneja Msaidizi chini ya Louis van Gaal.
Van Gaal, mwenye Miaka 63, ndio anamaliza Msimu wake wa kwanza na Man United na Mkataba wake unakwisha 2017.

Akihojiwa na MUTV, Kituo cha TV cha Man United, Van Gaal alisema: "Natarajia atakuwa Meneja anaefuata mimi nikiondoka. Kwa sasa mimi naongoza. Yeye anazo kazi za kufanya kama walivyo Wachezaji. Vitu ambavyo anapaswa kufanya chini yangu anavifanya vizuri sana! "

Giggs, mwenye Miaka 41, aliwahi kusema anasikia fahari kubwa kuiongoza Man United alipokabidhiwa madaraka mara baada ya kufukuzwa David Moyes.
Giggs ameichezea Man United tangu utoto wake na kuweka Rekodi ya kucheza Mechi 963 ambazo ni nyingi kupita Mchezaji mwingine yeyote.
Akiwa kama Kaimu Meneja Msimu uliopita, Giggs aliiongoza Man United kwa Mechi 4 ambazo alishinda Mechi 2, kupata Sare 1 na kufungwa 1.
Meneja wa Manchester United Louis van Gaal anaamini kuwa Klabu hiyo itamteua Ryan Giggs kama mrithi wake.

Msimu uliopita, Giggs aliiongoza Man United kwa Mechi 4 baada ya kutimuliwa David Moyes na Mwezi Mei akateuliwa kuwa Meneja Msaidizi chini ya Louis van Gaal.
Van Gaal, mwenye Miaka 63, ndio anamaliza Msimu wake wa kwanza na Man United na Mkataba wake unakwisha 2017.

Akihojiwa na MUTV, Kituo cha TV cha Man United, Van Gaal alisema: "Natarajia atakuwa Meneja anaefuata mimi nikiondoka. Kwa sasa mimi naongoza. Yeye anazo kazi za kufanya kama walivyo Wachezaji. Vitu ambavyo anapaswa kufanya chini yangu anavifanya vizuri sana! "
Giggs, mwenye Miaka 41, aliwahi kusema anasikia fahari kubwa kuiongoza Man United alipokabidhiwa madaraka mara baada ya kufukuzwa David Moyes.

Giggs ameichezea Man United tangu utoto wake na kuweka Rekodi ya kucheza Mechi 963 ambazo ni nyingi kupita Mchezaji mwingine yeyote.
Akiwa kama Kaimu Meneja Msimu uliopita, Giggs aliiongoza Man United kwa Mechi 4 ambazo alishinda Mechi 2, kupata Sare 1 na kufungwa 1.

No comments:

Post a Comment