BUKOBA SPORTS

Monday, April 20, 2015

MTANANGE WA YANGA vs STAND UNITED KUPIGWA KESHO JUMANNE TAIFA.

VPL KUENDELEA KESHO JUMANNE.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara inatarajiwa kuendelea kesho jumanne kwa mchezo mmoja katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, vinara wa ligi hiyo Young Africans watawakaribisha timu ya Stand United kutoka mjini Shinyanga.

Ligi hiyo itaendelea siku ya jumatano kwa michezo miwili, Simba SC watakuwa wenyeji wa Mgambo Shooting katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, huku Polisi Morogoro wakiwakaribisha Coastal Union katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

No comments:

Post a Comment