
Jumamosi JKT Ruvu watakua wenyeji wa Coastal Union katika Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es salaam, huku wakata miwa wa Kagera Sugar wakiwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Ligi hiyo itaendelea siku ya jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Young Africans watawakaribisha timu ya Mbeya City kutoka mkoani Mbeya, huku mjini Shinyanga katika uwanja wa Kambarage wenyeji timu ya Stand United wakiwakaribisha maafande wa timu ya Polisi Morogoro.
LIGI KUU VODACOM
RATIBA:
Jumamosi Aprili 11
JKT Ruvu vs Coastal Union
Kagera Sugar vs Ruvu Shooting
Mtibwa Sugar vs Azam FC
Ndanda FC vs Tanzania Prisons
Jumapili Aprili 12
Yanga vs Mbeya City
Stand United vs Polisi Moro
No comments:
Post a Comment