BUKOBA SPORTS

Saturday, May 2, 2015

LIVERPOOL 2 vs 1 QPR, KEPTENI STEVEN GERRARD AKOSA PENATI NA KUIPA USHINDI LIVERPOOL ANFIELD!

Steven G. akipongenzwa na MashabikiDakika ya 87 Steven Gerrard aliwafungia bao la Ushindi Liverpool na kufanya 2-1 dhidi ya QPR. Ushindi huo umewaacha nafasi ya 5 wakiwa na pointi 61. Queens Park Rangers wao wamebakia nafasi ya 19 wakiwa pointi 27.
Baada kukosa Penati iliyookolewa na Kipa, Kepteni wa Liverpool, Steven Gerrard, alifuta makosa yake na kuipa Bao la ushindi Liverpool walipoifunga Timu ambayo iko kwenye balaa kushushwa Daraja, QPR, Bao 2-1.
Liverpool, wakiwa kwao Anfield, walitangulia kufunga katika Dakika ya 19 kwa Bao la la Philippe Coutninho na QPR kusawazisha Dakika ya 73 Mfungaji akiwa Leroy Fer.
Liverpool walipewa Penati Dakika ya 79 na Gerrard kuikosa na kisha Dakika ya 82 QPR kubaki Mtu 10 baada ya Nedum Ohuoha kupewa Kadi za Njano 2 ndani ya Dakika 3 tu na kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
Dakika ya 87, Gerrard akafunga Bao la ushindi kwa Liverpool na kuweka hai matumaini yao finyu ya kufuzu 4 Bora wakiwa Nafasi ya 5 Pointi 4 nyuma ya Man United wenye Mechi 1 mkononi huku Liverpool wakibakiza Mechi 3.

Leroy Fer of QPR celebrates scoring his goal to make it 1-1 with a message on his shirt for Rio Ferdinand and his familyLeroy Fer wa Queens Park Rangers aliwasawazishia bao QPR na kufanya 1-1Philippe Coutinho dakika ya  19 kipindi cha kwanza alifunga bao.

No comments:

Post a Comment