Jambo Bukoba ni Shirika lisilokuwa la Serikali linalofanya kazi mkoani Kagera kwa kushirikiana na serikali ya Mkoa.
Mwanzilishi wa Jambo Bukoba ni Bw. Clemence Mlokozi ambaye asili yake ni Mkoani Kagera katika Wilaya ya Missenyi Kijiji Ishozi na anaishi nchini Ujerumani.
Jambo Bukoba ilianzishwa Mkoani Kagera kwa kusaidia watoto hasa wanafunzi wa shule za msingi kuanzia miaka 5 hadi 19 kujenga afya zao kimichezo ili kujikinga na Maabukizi ya UKIMWI, kuweka haki sawa katika elimu kupitia michezo kwa wasichana na wavulana.
Shirika hili chini ya mwanzilishi wake Bw. Mulokozi tangu kuanzishwa kwake mkoani Kagera limekuwa likiwafunza watoto katika shule za msingi kila wilaya michezo midogo midogo ya kujenga ushirikiano wa pamoja hasa watoto wa kike kujiamini na kushirikiana zaidi na wenzao wa kiume.
Walimu hao ni Peace Saleand kutoka Biharamulo- Rubondo Shule ya Msingi. Grace Wamara kutoka Shule ya Msingi Tumaini ambayo Ipo Bukoba Mjini. Alistidia Bijura kutoka Shule ya msingi Kaisho - Kyerwa.
Elizabeth John kutoka Rulenge Shule msingi - Ngara
Abela Ndeyokobora Kutoka Shule ya Msingi Kayanga - Karagwe
Jeni Mulokozi Kutoka kashekya Shule ya Msingi - Misenyi
William Magosa kutoka Karalo Shule ya Msingi -Karagwe
No comments:
Post a Comment