BUKOBA SPORTS

Sunday, June 14, 2015

KINANA AITAKA SERIKALI KURAHISISHA UTOAJI WA LESENI KWA WAFANYABIASHARA,MADEREVA WA MAGARI NA BODABODA


Wananchi wa Ngara mjini wakishangilia jambo katika mkutano wa hadhara wa CCM

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa mji wa Ngara Mjini kwenye mkutano wa hadara,Nape Nnauye alisema kuwa hakuna sababu ya Watanzania kuingia kwenye mpasuko kwa sababu ya mchakato wa katiba mpya na kuashauri ni vema mjadala ukafungwa kwenye nyumba za ibada. Amesema inasikitisha unapoona baadhi ya viongozi wa dini badala ya kuhubiri neno la Mungu na kuwaunganisha Watanzania wanatumia nafasi yao kuwagawa wananchi kwa sabababu ya Katiba mpya.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Abdulrhaman Kinana akiwahutubia wananchi wa Ngara mjini,Kinana ameitaka Serikali kurahisisha utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara , madereva wa magari na bodaboda badala ya kuacha watu wanasumbuka kutafuta leseni umbali mrefu tena kwa gharama kubwa.

Kinana amesema kuwa moja ya ombi la wananchi hao ilikuwa ni kuomba kurahisishiwa kupata leseni ili kuondoa usumbufu wanaoupata sasa.Alisema Serikali lazima iweke mazingira mazuri ya kutoa leseni kwa wananchi wakiwamo wafanyabishara na madereva bodaboda huku akieleza hakuna sababu ya kutumia gharama kubwa kwa ajili ya leseni.

Sehemu ya wananchi waliohudhuria mkutano huo


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua rasmi Chanjo ya watoto kuzuia maambukizi ya magonjwa katika kata ya Nyakisasa kijiji cha Kashinga akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Ngara mkoani Kagera,lengo la ziara hiyo likiwani ni kukagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010 na kuhimiza uhai wa chama, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na ktibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na viongozi mbalimbali wa CCM kutoka mkoa wa Kagera.

Baadhi ya akina mama na watoto wao wakisubiri watoto wao kupatiwa chanjo katika zahanati ya kijiji cha Kashinga wilayani Ngara.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi hawapo pichani wakati alipozindua chanjo ya watoto katika zahanati ya Kashinga akiwa katika ziara ya kikazi wilayani Ngara leo wa tatu kutoka kulia ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM na katikati ni Mkuu wa mkoa wa Kagera Mh. John Mongella

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti wa kumbukumbu katika zahanati hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na viongozi wa CCM wilayani Ngara wakishiriki kwa pamoja katika ujenzi wa ofisi ya CCM tawi la Munjebwe, Rulenge.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Rulenge.

Baadhi ya Wafuasi wa chama cha CHADEMa wakikabidhi kadi zao kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana,na kutangaza kujiunga na chama chama CCM.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi mbalimbali za waliokuwa wanachama wa Chama cha CHADEMA mara baada ya kurejesha kwake na kujiunga na CCM katika mji wa Rulenge.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ngara Mama Constansia Buhie wakizikusanya kadi mbalimbali za wafuasi wa upinzani na kuzikabidhi kwa viongozi hao wa CCM,ikiwa ni ishara ya kujiunga na chama hicho cha CCM

Baadhi ya kadi zilizorejeshwa kwa Kinana na wananchi hao na kujiunga na CCM.

Kwaya ya akina mama wa Rulenge wakiimba wimbo maalum wakati wa mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mzee Godwin Magambo wakati alipowasilisha malalamiko yake ya ardhi

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mhandisi wa kampuni ya kichina ya TKPE Bw.Ton Minyang wakati alipokagua ujenzi wa Mtambo wa umeme vijijini REA unaojengwa katika kijiji cha Djuruligwa kata ya Kabanga wilayani Ngara.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua kkikundi cha akina mama wajasiriamali cha mjini Ngara kabla ya kuhutubia mkutano wake na wananchi mjini humo leo.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata keki kuashiria uzinduzi wa kikundi hicho cha akina mama wajasiriamali.

No comments:

Post a Comment