Kerr aliyasema hayo baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na kulakiwa na wajumbe wa Kamati ya Simba, Collin Frisch na Said Tully.
“Nimefurahi kuja Tanzania na nawaahidi viongozi na mashabiki kuwa nitahakikisha naendeleza wachezaji chipukizi hili Simba iweze kutamba sasa na baadae”, alisema Kerr.
Kocha huyo ambaye amerithi mikoba ya Mserbia Goran Kopunovic amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha Simba ambapo atakuwa anasaidiwa na kiungo wa zamani wa timu hiyo Suleman Matola.
Simba waliamua kuachana na Kopunovic na kusaka kocha huyo mpya baada ya Mserbia huyo kuhitaji Simba imlipe kiasi cha Dola za Marekani 50,000 (sh. Milioni 100) kama ada ya usajili na mshahara wake ambapo kila mwezi atakuwa analipwa dola za Marekani 14,000 9sh. Milioni 28).
Dylan Kerr mwenye umri wa miaka 47, aliwahi kuwa mchezaji, alicheza beki wa kulia kwenye klabu za Leeds United, Reading, Blackpool na nyingine nyingi za Uingereza huku akihudumu kama kocha msaidizi kwenye timu mbalimbali katika nchi za Vietnam ambako ametoka kwenye timu ya Hai Phong F.C. ambako alimaliza mkataba 2014.
No comments:
Post a Comment