BUKOBA SPORTS

Sunday, June 21, 2015

COPA AMERICA: ARGENTINA 1 vs 0 JAMAICA, GONZALO HIGUAIN AITUNGUA JAMAICA, WASONGA ROBO FAINALI!!

Gonzalo Higuaín dakika ya 11 kipindi cha kwanza aliifungia bao Argentina baada ya kupata pasi kutoka kwa Angel Di Maria.Kipindi cha pili Timu hizo pamoja na kucheza kwa kasi hakuna Timu iliyoziona nyavu za mpinzani wake mpaka dakika 90  zinamalizika Argentina ndio walikuwa kidedea kwa Ushindi wa bao 1-0.
Lionel Messi kulia akiachia shuti kali.
Nao Mabingwa Watetezi Uruguay wametinga Robo Fainali za Copa America kwa Tiketi ya moja ya Timu mbili zilizofuzu Nafasi ya 3 Bora katika Kundi lao baada ya kutoka Sare 1-1 na Paraguay ambao wameshika Nafasi ya Pili ya Kundi B.
Argentina, ambao Jana waliitungua Jamaica, Timu ambayo ni Wageni Waalikwa wa Mashindano haya, Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 11 la Gonzalo Higuian, wao wameshika Nambari Wani Kundi B.
Katika Mechi ya Uruguay na Paraguay, Bao la Dakika ya 29 la Jose Maria Gimenez liliwapa Uruguay uongozi lakini Dakika ya 44 Lucas Barrios aliisawazishia Paraguay.

Lionel Messi ndie Nahodha

No comments:

Post a Comment