Said Mohamed ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya TFF, aliyasema hayo jana wakati akifungua kozi ya makocha wa golikipa inayoendelea katika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Naye mshiriki Mohamed Mwameja ‘Tanzania One’ ambaye amewahi kuidakia Simba na timu ya Taifa alishukuru kupata kozi hiyo na kusema itawasaidia kujua makosa yao kwani wamekuwa wakifundisha kwa uzoefu ambao waliupata wakati wakicheza.
Jumla ya makocha 31 wanashiriki kozi hiyo kutoka vilabu vyote viliyovopo Ligi Kuu ya Tanzania Bara na Zanzibar na magolikipa wa zamani walio wahi kudaka timu za Taifa.
Kozi hiyo inaendeshwa na mkufunzi wa FIFA Elaxander kutoka nchini Ufaransa, ambaye alidumu kama golikipa kwa miaka 20 na inatarajiwa kufungwa Julai 17, mwaka huu
No comments:
Post a Comment