Romero, mwenye Miaka 28, Msimu uliopita alikuwa kwa Mkopo huko AS Monaco kutoka Sampdoria na kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwaka Jana, Kipa huyo aling'ara alipokuwa Namba Wani wa Argentina iliyofika Fainali na kufungwa 1-0 na Germany.
Hata hivyo, AS Roma nayo pia inamtaka Romero ambae sasa ni Mchezaji Huru baada ya Mkataba wake na Sampdoria kumalizika.
Van Gaal anamtaka Romero kuziba pengo la Valdés ambae alikwaruzana nae kwa kugomea kuchezea Kikosi cha Pili cha Man United na hilo kumfanya asichukuliwe kwenye Ziara ya sasa huko Marekani.

Hata hivyo, Sergio Romero anatarajiwa kuwa Kipa Namba Mbili nyuma ya Kipa yeyote atakaembadili De Gea, ikiwa ataondoka, huku Kipa wa Ajax na Timu ya Taifa ya Holland, Jasper Cillessen, akitajwa kuwa ndie mrithi wa De Gea.
No comments:
Post a Comment