BUKOBA SPORTS

Monday, September 14, 2015

USIKU WA UEFA CHAMPIONS LIGI KUANZA JUMANNE NA JUMATANO. MAN CITY vs JUVENTUS, PSV EINDHOVEN vs MAN UNITED, GALATASARAY vs ATLETICO MADRID, JUMATANO CHELSEA UWANJANI!

Kepteni wa Manchester United Wayne Rooney kuikosa Mechi ya ufunguzi ya Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, hapo Jumanne.
Rooney, ambae pia ni Kepteni wa England, hakucheza Jumamosi wakati Man United inaifunga Liverpool 3-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
Jumanne Man United wanasafiri kwenda Nchini Netherlands kucheza na Mabingwa wao PSV Eindhoven katika Mechi ya Kwanza ya Kundi B la UCL.
Jana Meneja wa Man United Louis van Gaal alidokeza kuwa huenda Rooney asicheze Mechi hii kutokana na matatizo ya Musuli za Pajani.

Kukosekana kwa Rooney huenda kukatoa mwanya kwa Chipukizi mpya kutoka France Anthony Martial kuanza Mechi yake ya kwanza kwa Man United.
Jumamosi Martial alitoka Benchi na kuifungia Man United Bao murua la 3 wakati Man United wanaichapa Liverpool 3-1.
Mchezaji mwingine mvuto kwenye Mechi hii ni Memphis Depay alienunuliwa na Man United kutoka PSV mwanzoni mwa Msimu huu.
Msimu uliopita Memphis ndie aliekuwa Mfungaji Bora huko Netherlands na kuibeba PSV kutwaa Ubingwa.

UEFA CHAMPIONS LIGI
Mechi za Makundi
Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku
Jumanne Septemba 15

Man City vs Juventus
PSV Eindhoven vs Man United
Real Madrid vs FC Shakhtar Donetsk
Sevilla vs Borussia Monchengladbach
VfL Wolfsburg vs CSKA Moscow
PSG vs Malmo Ff
Galatasaray vs Atletico Madrid
Benfica vs FC Astana

Jumatano Septemba 16
Chelsea vs Maccabi Tel Aviv
AS Roma vs Barcelona
Valencia vs Zenit St Petersburg
Bayer Leverkusen vs FC BATE Borisov
FC Dynamo Kiev vs FC Porto
Olympiacos vs Bayern Munich
NK Dinamo Zagreb vs Arsenal
KAA Gent vs Lyon

No comments:

Post a Comment